Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Simba waja na ‘Iga Ufe’
Michezo

Simba waja na ‘Iga Ufe’

Spread the love

KLABU ya Simba imezindua wiki yao rasmi kuelekea kilele cha tamasha lao la ‘Simba Day’ kitakachofanyika tarehe 6, Agosti 2019 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku wakiwa na kauli mbiu ya ‘Iga ufe’. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Msemaji wa klabu hiyo Haji Manara amesema tamasha hilo ni la mwaka wa 10 sasa toka 2009 na kuonesha mafanikio makubwa huku baadhi ya klabu zikiiga utamadui huo.

“Tumefanya hili tamasha huu ni mwaka wa 10 mfululizo, toka enzi za Mzee Dalali (Hassan) na Kaduguda (Mwina), na matarajio yetu hili jambo litakuwa endelevu kwa miaka yote ya uhai wa simba na jambo jema lazima liigwe,” alisema Manara.

Kuelekea kilele cha tamasha hilo Simba itarajia kufanya shughuli mbalimbali ndani ya wiki hii kama kuzindua jezi, kuwatembelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu, kuwatembelea wagonjwa hospitali sambamba na uchangiaji wa damu.

Siki hiyo pia Simba itarajia kutambulisha kikosi chao cha wachezaji na benchi la ufundi watakaotumika kwenye msimu wa ligi wa 2019/2020 sambamba na michuano ya klabu bingwa Afrika na kucheza mchezo wa kirafiki na klabu ya Power Dynamos kutoka Zambia

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!