Friday , 19 April 2024
Home Kitengo Michezo Simba waja na ‘Iga Ufe’
Michezo

Simba waja na ‘Iga Ufe’

Spread the love

KLABU ya Simba imezindua wiki yao rasmi kuelekea kilele cha tamasha lao la ‘Simba Day’ kitakachofanyika tarehe 6, Agosti 2019 katika Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam, huku wakiwa na kauli mbiu ya ‘Iga ufe’. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Msemaji wa klabu hiyo Haji Manara amesema tamasha hilo ni la mwaka wa 10 sasa toka 2009 na kuonesha mafanikio makubwa huku baadhi ya klabu zikiiga utamadui huo.

“Tumefanya hili tamasha huu ni mwaka wa 10 mfululizo, toka enzi za Mzee Dalali (Hassan) na Kaduguda (Mwina), na matarajio yetu hili jambo litakuwa endelevu kwa miaka yote ya uhai wa simba na jambo jema lazima liigwe,” alisema Manara.

Kuelekea kilele cha tamasha hilo Simba itarajia kufanya shughuli mbalimbali ndani ya wiki hii kama kuzindua jezi, kuwatembelea watoto wanaoishi katika mazingira magumu, kuwatembelea wagonjwa hospitali sambamba na uchangiaji wa damu.

Siki hiyo pia Simba itarajia kutambulisha kikosi chao cha wachezaji na benchi la ufundi watakaotumika kwenye msimu wa ligi wa 2019/2020 sambamba na michuano ya klabu bingwa Afrika na kucheza mchezo wa kirafiki na klabu ya Power Dynamos kutoka Zambia

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Piga pesa na mechi za EUROPA leo hii

Spread the love Hatimaye Alhamisi ya EUROPA imefika ambapo leo hii mechi...

Michezo

Leo ni leo nani kutinga nusu fainali UEFA?

Spread the love HATIMAYE Jumanne ya UEFA imefika ambapo leo hii michezo...

Michezo

Anza Jumatatu yako na Meridianbet

Spread the love  IKIWA ni siku nyingine mpya kabisa ya Jumatatu baadhi...

Habari MchanganyikoMichezo

NBC, Yanga wazindua kadi  za kimataifa za uanachama

Spread the loveBenki ya Taifa ya Biashara (NBC) kwa kushirikiana na Klabu...

error: Content is protected !!