Friday , 29 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwandishi Erick Kabendera, azingirwa nyumbani kwake
Habari Mchanganyiko

Mwandishi Erick Kabendera, azingirwa nyumbani kwake

Spread the love

MWANDISHI wa habari za kiuchunguzi, Erick Kabendera, amevamiwa na “watu wasiojulikana,” nyumbani kwake Mbweni, jijini Dar es Salaam. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa Kabendera, leo jioni watu kadhaa wakiwa na magari, walivamia nyumbani kwake na kuzingira nyumba hiyo na kuzuia mtu yeyote kuingia.

Anasema, kabla ya hapo, simu zake zote zilifungwa; na alipopiga simu Vodacom aliambiwa kuwa hayo ndio maelekezo waliyopewa na Mamlaka ya Mawasiliano ya taifa (TCRA).

Naye mtoa taarifa mmoja ameliambia MwanaHALISI ONLINE, kwamba “…inawezekana wamemchukua tayari; sababu hata simu za ndani ya nyumba hazipokelewi.”

Kabendera ni mmoja wa waandishi wa habari nchini anayeandikia magazeti mbalimbali, likiwamo gazeti la Africa Confidential linalochapishwa Uingereza.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

DAWASA waanza utekelezaji agizo la Samia

Spread the loveMamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam...

Habari MchanganyikoKimataifa

Zuma akataliwa kugombea urais

Spread the loveTUME Huru ya Uchaguzi Afrika Kusini (IEC) imemwondoa rais wa...

Habari Mchanganyiko

Mtandao watetezi wa haki za mazingira Tanzania waundwa

Spread the loveMTANDAO wa watetezi wa haki za mazingira nchini Tanzania, umeundwa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga kuongoza usambazaji wa mitungi ya gesi 10,000 ya Taifa Gas

Spread the loveNaibu Waziri wa Nishati, Judith Kapinga ameahidi kuongoza kwa ufanisi...

error: Content is protected !!