Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Wachafukoga marufuku kuingia mjini-Makonda
Habari Mchanganyiko

Wachafukoga marufuku kuingia mjini-Makonda

Spread the love

WATANZANI wachafu wamepigwa marufuku kuonekana mijini hususani katika kipindi hiki cha Mkutano wa Nchi Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Marufuku hiyo imetolewa na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam leo tarehe 29 Julai 2019, kwenye uzinduzi wa kampeni ya usafi wa jiji hilo.

Kampeni hiyo imezinduliwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano huo wa 39. Mkutano huo unatarajiwa kufanyika kwa siku mbili, kuanzia tarehe 18 hadi 19 Agosti 2019.

Makonda amepiga marufuku ya kuingia katika viunga vya mjini na nguo zisizonyooshwa “tabia ya kuna mjini bila kunyoosha nguo ni marufuku,” na kuongeza “tabia ya kuja mjini hujaoga ni aibu.”

Kiongozi huo wa Dar es Salaam pia ameonya watu wenye tabia za kwenda mjini bila kuwa wasafi, na kwamba ni bora wasubiri mkutano huo upite.

“Watu wanatembea tu na chawa, kama huwezi kuwa msafi basi subiri mwezi huu upite…”kama hufui nguo, kama huogi, pumzika kidogo kuja mjini, kwa kipindi hiki tuvumiliane,” amesema.

Katika kampeni hiyo Makonda ameshauri kwamba, dereva yeyote atakayekamatwa anatupa takataka asitozwe faini na badala yake apewe eneo la kufanya usafi.

Kwenye harakati hizo Makonda amesema, anafanya hivyo kwa kuwa hataki kumtia aibu mkuu wa nchi, Rais John Magufuli ambaye ndiye mwenyeji wa mkutano huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!