Friday , 26 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Wachafukoga marufuku kuingia mjini-Makonda
Habari Mchanganyiko

Wachafukoga marufuku kuingia mjini-Makonda

Spread the love

WATANZANI wachafu wamepigwa marufuku kuonekana mijini hususani katika kipindi hiki cha Mkutano wa Nchi Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC). Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Marufuku hiyo imetolewa na Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam leo tarehe 29 Julai 2019, kwenye uzinduzi wa kampeni ya usafi wa jiji hilo.

Kampeni hiyo imezinduliwa ikiwa ni sehemu ya maandalizi ya mkutano huo wa 39. Mkutano huo unatarajiwa kufanyika kwa siku mbili, kuanzia tarehe 18 hadi 19 Agosti 2019.

Makonda amepiga marufuku ya kuingia katika viunga vya mjini na nguo zisizonyooshwa “tabia ya kuna mjini bila kunyoosha nguo ni marufuku,” na kuongeza “tabia ya kuja mjini hujaoga ni aibu.”

Kiongozi huo wa Dar es Salaam pia ameonya watu wenye tabia za kwenda mjini bila kuwa wasafi, na kwamba ni bora wasubiri mkutano huo upite.

“Watu wanatembea tu na chawa, kama huwezi kuwa msafi basi subiri mwezi huu upite…”kama hufui nguo, kama huogi, pumzika kidogo kuja mjini, kwa kipindi hiki tuvumiliane,” amesema.

Katika kampeni hiyo Makonda ameshauri kwamba, dereva yeyote atakayekamatwa anatupa takataka asitozwe faini na badala yake apewe eneo la kufanya usafi.

Kwenye harakati hizo Makonda amesema, anafanya hivyo kwa kuwa hataki kumtia aibu mkuu wa nchi, Rais John Magufuli ambaye ndiye mwenyeji wa mkutano huo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!