Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Mbatia apewa miaka mitano NCCR-Mageuzi
Habari za Siasa

Mbatia apewa miaka mitano NCCR-Mageuzi

Spread the love

JAMES Mbatia, amechaguliwa tena kuwa Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi huku Angelina John, akichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Bara na Ambar Hamis ameukwaa umakamu mwenyekiti visiwani Zanzibar. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Florian Mbeo, mkuu wa oganaizesheni na utawala wa chama hicho amesema, Mbatia na timu yake itaongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo kwa mujibu wa katiba yao.

Mkutano wa chama hicho leo tarehe 28 Julai 2019 pia umechagua wajumbe wa halmashauri kuu ambapo Mbeo amesema, kwa mujibu wa katiba yao, anapotokea mgombea mmoja kwenye nafasi, basi hupiga kura za ndio ama hapana.

Akifafanua namna Mbatia alivyopita na kuendelea kuongoza chama hicho amesema, katika nafasi ya uenyekiti alijitokeza yeye (Mbatia) peke yake ambapo alipigiwa kura za ndio 201 huku tisa zikimkataa.

“Kwa mujibu wa matokeo hayo, Mhe Mbatia atakuwa mwenyekiti wetu kwa miaka mitango mingine ijayo,” amesema Mbeo na kuongeza “viongozi wengine wanaendelea kuchaguliwa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!