Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mbatia apewa miaka mitano NCCR-Mageuzi
Habari za Siasa

Mbatia apewa miaka mitano NCCR-Mageuzi

Spread the love

JAMES Mbatia, amechaguliwa tena kuwa Mwenyekiti wa Chama cha NCCR-Mageuzi huku Angelina John, akichaguliwa kuwa Makamu Mwenyekiti Bara na Ambar Hamis ameukwaa umakamu mwenyekiti visiwani Zanzibar. Anaripoti Faki Sosi…(endelea).

Florian Mbeo, mkuu wa oganaizesheni na utawala wa chama hicho amesema, Mbatia na timu yake itaongoza chama hicho kwa miaka mitano ijayo kwa mujibu wa katiba yao.

Mkutano wa chama hicho leo tarehe 28 Julai 2019 pia umechagua wajumbe wa halmashauri kuu ambapo Mbeo amesema, kwa mujibu wa katiba yao, anapotokea mgombea mmoja kwenye nafasi, basi hupiga kura za ndio ama hapana.

Akifafanua namna Mbatia alivyopita na kuendelea kuongoza chama hicho amesema, katika nafasi ya uenyekiti alijitokeza yeye (Mbatia) peke yake ambapo alipigiwa kura za ndio 201 huku tisa zikimkataa.

“Kwa mujibu wa matokeo hayo, Mhe Mbatia atakuwa mwenyekiti wetu kwa miaka mitango mingine ijayo,” amesema Mbeo na kuongeza “viongozi wengine wanaendelea kuchaguliwa.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

Habari za SiasaTangulizi

Mgawo wa umeme: Rais Samia ampa miezi sita bosi mpya TANESCO

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amempa miezi sita Mkurugenzi...

Habari za Siasa

Rais Samia avunja bodi ya REA

Spread the loveRAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amemteua Balozi Jacob Kingu, kuwa...

error: Content is protected !!