Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Kifo cha mhandisi Z’bar, giza nene
Habari Mchanganyiko

Kifo cha mhandisi Z’bar, giza nene

Spread the love

HAJI Abdallah Khatib, Mhandisi msaidizi wa meli ya MV Mapinduzi, amefariki dunia kwa kujinyonga ndani ya meli hiyo. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumzia kifo hicho kilichotokea leo tarehe 22 Julai 2019, Mustafa Aboud Juma, Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano na Usafirishaji visiwani Zanzibar amesema, mpaka sasa hakuna taarifa zozote za chanzo cha kifo hicho.

“Hatujajua chochote mpaka sasa, hatuelewi sababu za kujinyonga,” amesema Juma.

Mhandisi huyo alijinyonga wakati meli hiyo ikitoka Unguja kwenda Pemba na kwamba, baada ya taarifa za kifo hicho, meli hiyo ilisitisha kuendelea na safari na kurudishwa Unguja.

Taarifa zaidi zinaeleza, Injinia Khatib (55) alijinyonga akiwa kwenye chumba cha injini ambamo ndio muda wote hufanyia kazi zake.

Akizungumzia utendaji wa injinia huo, Juma amesema injinia huo alikuwa ni mzowefu na aliyefanya kazi hizo kwa muda mrefu na weledi mkubwa.

Hata hivyo ameeleza, Jeshi la Polisi visiwani humo limeanza kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!