Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Kifo cha mhandisi Z’bar, giza nene
Habari Mchanganyiko

Kifo cha mhandisi Z’bar, giza nene

Spread the love

HAJI Abdallah Khatib, Mhandisi msaidizi wa meli ya MV Mapinduzi, amefariki dunia kwa kujinyonga ndani ya meli hiyo. Anaandika Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumzia kifo hicho kilichotokea leo tarehe 22 Julai 2019, Mustafa Aboud Juma, Katibu Mkuu Wizara ya Mawasiliano na Usafirishaji visiwani Zanzibar amesema, mpaka sasa hakuna taarifa zozote za chanzo cha kifo hicho.

“Hatujajua chochote mpaka sasa, hatuelewi sababu za kujinyonga,” amesema Juma.

Mhandisi huyo alijinyonga wakati meli hiyo ikitoka Unguja kwenda Pemba na kwamba, baada ya taarifa za kifo hicho, meli hiyo ilisitisha kuendelea na safari na kurudishwa Unguja.

Taarifa zaidi zinaeleza, Injinia Khatib (55) alijinyonga akiwa kwenye chumba cha injini ambamo ndio muda wote hufanyia kazi zake.

Akizungumzia utendaji wa injinia huo, Juma amesema injinia huo alikuwa ni mzowefu na aliyefanya kazi hizo kwa muda mrefu na weledi mkubwa.

Hata hivyo ameeleza, Jeshi la Polisi visiwani humo limeanza kufanya uchunguzi ili kubaini chanzo cha kifo hicho.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!