Sunday , 28 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amtimua uwaziri January Makamba
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli amtimua uwaziri January Makamba

Spread the love

RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo tarehe 21 Julai 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa, George Simbachawene ameteuliwa na Rais Magufuli kuirithi mikoba ya January kuanzia siku ya leo.

Aidha, taarifa hiyo imeeleza kwamba, Rais Magufuli amemteua Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, akichukua nafasi ya Innocent Bashungwa, aliyeteuliwa hivi karibuni kuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Magufuli amemteua Balozi, Dk. Martin Lumbanga kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA).

https://twitter.com/jmakamba/status/1152798935355985922?s=21

Muda mchache baada ya kuvuliwa Uwaziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira na Rais John Magufuli, January Makamba atoa neno.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, leo tarehe 21 Julai 2019, January amesema ameyapokea mabadiliko hayo, kwa moyo mweupe.

Aidha, January amesema atazungumza zaidi siku zijazo, inagawa hakuweka bayana suala gani atakalolizungumzia.

“Kwa kweli nimeyapokea mabadiliko yaliyofanywa kwa moyo mweupe kabisa kabisa 😊. Nitasema zaidi siku zijazo,” ameandika January katika ukurasa wake wa Twitter.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

error: Content is protected !!