Thursday , 28 March 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Rais Magufuli amtimua uwaziri January Makamba
Habari za SiasaTangulizi

Rais Magufuli amtimua uwaziri January Makamba

Spread the love

RAIS John Magufuli ametengua uteuzi wa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira, January Makamba. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo tarehe 21 Julai 2019 na Mkurugenzi wa Mawasiliano ya Rais Ikulu, Gerson Msigwa.

Taarifa ya Msigwa inaeleza kuwa, George Simbachawene ameteuliwa na Rais Magufuli kuirithi mikoba ya January kuanzia siku ya leo.

Aidha, taarifa hiyo imeeleza kwamba, Rais Magufuli amemteua Mbunge wa Nzega, Hussein Bashe kuwa Naibu Waziri wa Kilimo, akichukua nafasi ya Innocent Bashungwa, aliyeteuliwa hivi karibuni kuwa Waziri wa Viwanda, Biashara na Uwekezaji.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo, Rais Magufuli amemteua Balozi, Dk. Martin Lumbanga kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi ya Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA).

https://twitter.com/jmakamba/status/1152798935355985922?s=21

Muda mchache baada ya kuvuliwa Uwaziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na Mazingira na Rais John Magufuli, January Makamba atoa neno.

Kupitia ukurasa wake wa Twitter, leo tarehe 21 Julai 2019, January amesema ameyapokea mabadiliko hayo, kwa moyo mweupe.

Aidha, January amesema atazungumza zaidi siku zijazo, inagawa hakuweka bayana suala gani atakalolizungumzia.

“Kwa kweli nimeyapokea mabadiliko yaliyofanywa kwa moyo mweupe kabisa kabisa 😊. Nitasema zaidi siku zijazo,” ameandika January katika ukurasa wake wa Twitter.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Nani anasema kuna hasara ATCL?

Spread the loveRIPOTI za makusanyo na matumizi ya fedha katika Kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

CAG: Wastaafu, wenza wao chanzo NHIF kufilisika

Spread the loveRIPOTI ya ukaguzi ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu...

Habari za SiasaTangulizi

Vikundi hewa 851 vyalamba bilioni 2.6 mikopo ya halmashauri

Spread the loveVIKUNDI hewa vya wajasirimali wadogo 851 kutoka katika halmashauri 19...

Habari za SiasaTangulizi

Mashirika matano yapata hasara mabilioni ya fedha

Spread the loveMASHIRIKA matano ya Serikali yanayojiendesha kibiashara, yamepata hasara ya mabilioni...

error: Content is protected !!