Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Tuhuma nzito ziara ya Rais Magufuli
Habari za Siasa

Tuhuma nzito ziara ya Rais Magufuli

Spread the love

ZIARA ya Rais John Magufuli katika gereza kuu la Butimba jijini Mwanza, imeibua tuhuma nzito. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Kalikenya Nyamboge, mfungwa anayetumikia kifungo cha miaka 30 kwenye gereza hilo, mbele ya Rais Magufuli ameibua kwamba, gerezaji hapo ukichomwa sindano, unakufa huku wengine kuporwa mali na maofisa wa gereza hilo.

Hata hivyo, amemweleza rais kuwa, kwa sasa vifo vya wafungwa vimepungua baada ya Jenerali Kamishna (hakumtaja jina) kupeleka mganga msomi mpya.

“Na si mara ya kwanza wao kuua mimi nilikuwa nimepanga nikitoka nije kukwambia na nikitoka nitakuletea mambo yote yanayotokea huku, lakini huyu usimuache maana kwa Mwenyezi Mungu utakua umeandika maelezo ya mauji,” amenukuliwa Nyamboge.

Mfungwa huyo anamthibitishia Rais Magufuli kwamba, kwenye gereza hilo, vitendo vya ajabu vimekuwa vikifanywa na maofisa wa magereza.

Akizungumza madhila gereza hilo, Nyamboge amemtaja ofisa wa usalama wa gereza hilo kuwa kikwazo na mnyanyasaji akidai kuwa, huwapa wafungwa simu kisha wakikutwa nazo baada ya msako huporwa kila kitu.

Akizungumzia wasiwasi wa usalama wake Nyamboge amemwomba Rais Magufuli kuondoka na ofisa huyo kwa kuwa, anaweza kumdhuru endapo atamwacha.

“Mheshimiwa rais, huyu ofisa akupe mihuri na hizo simu uondoke nazo, utajua mwenyewe utaenda kufanyia nini na ikibidi ondoka naye kwani ukifanya hivyo utakiwa umetusaidia sana na ukimuacha atanidhuru,” amesema Nyamboge.

Rais Magufuli yupo ziarani Mwanza ambapo leo tarehe 16 Julai 2019, ametembelea gerezani kuu la Butimba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaKimataifa

Mwanamke Rwanda ataka kupambana tena na Kagame

Spread the loveKIONGOZI wa kihistoria wa upinzani nchini Rwanda, Victoire Ingabire Umuhoza,...

Habari za Siasa

Wizara ya Kilimo yapanga kutumia Sh. 1.2 trilioni 2024/25

Spread the loveWIZARA ya Kilimo, imepanga kutumia bajeti ya Sh. 1.2 trilioni...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

error: Content is protected !!