Saturday , 27 April 2024
Home Kitengo Michezo Wema Sepetu adakwa tena, atupwa rumande
Michezo

Wema Sepetu adakwa tena, atupwa rumande

Wema Sepetu (mwenye gauni jeusi) akitolewa mahakamani na kupelekwa mahabusu
Spread the love

WEMA Sepetu, Mwigizaji na Mshindi wa Mashindano ya Urembo mwaka 2006, amekamatwa tena leo tarehe 4 Julai 2019 na Jeshi la Magereza muda mchache baada ya mahakama kumwacha huru. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, jijini Dar es Salaam aliamua kumwacha huru Wema kutokana na upande wa mashtaka kushindwa kupeleka ushahidi.

Hata hivyo, wakili wa Wema – Albert Msando alilalamikia hatua ya Jamhuri kushindwa kupeleka ushahidi huku ikitoa visingizio mara kwa mara.  

Hakimu Maira Kasonde amemwacha huru Wema ambapo kwa mujibu wa Kifungu cha 225 (5) cha Mwenedno wa Makosa ya Jinai, kinatoa mwanya kwa Jamhuri kumkamata tena na kumfungulia upya mashtaka.

 Gloria Mwenda, Wakili wa Serikali mbele ya hakimu leo tarehe 4 Julai 2019, aliieleza mahakama kuwa, shauri hilo lilikuja kwa ajili ya kusikilizwa lakini shahidi waliokuwa wakimtegemea, wamepewa taarifa kuwa anaumwa.

Kauli hiyo ilipingwa na Wakili wa Wema ambapo alidai kuwa, taarifa ya wakili wa serikali haijajitosheleza huku akihoji siku ambayo muhusika alianza kuumwa. Amedai kuwa, taarifa hiyo ilitakiwa ijitosheleze.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Jumamosi ya leo ni ya pesa tu kutoka Meridianbet

Spread the love  IKIWA leo hii ni Jumamosi nyingine na tulivu kabisa,...

Michezo

EPL, Ligue 1 na Coppa Italia kinawaka leo

Spread the love  LEO ligi kadhaa zitaendelea nchini barani ulaya ikiwemo ligi...

BiasharaMichezo

NBC yaunga mkono jitihada kutokomeza malaria

Spread the loveKuelekea Maadhimisho ya siku ya malaria Duniani yatakayofanyika kesho Aprili...

Michezo

Arsenal dhidi ya Chelsea ngoma nzito leo EPL

Spread the love  Leo kutakua na mchezo mkali sana pale kwenye ligi...

error: Content is protected !!