Sunday , 28 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Buguruni, Ilala, Kinondoni, Mwenge kushuhudia mwili wa Dk. Mengi
Habari MchanganyikoTangulizi

Buguruni, Ilala, Kinondoni, Mwenge kushuhudia mwili wa Dk. Mengi

Spread the love

MWILI wa Dk. Reginald Abraham Mengi, aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni zilizo chini ya IPP Group, unatarajiwa kuletwa leo saa 8:30 mchana. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Usalama umeimarishwa katika sehemu mbalimbali, hususan maeneo mwili huo utapitishwa baada ya kufikishwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalim Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam kutoka Dubai, Falme za Kiarabu.

Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amezungumza na wananchi na kueleza barabara ambayo mwili huo utapitishwa pale utapoanza safari kutoka JNIA saa 9:45.

Barabara hizo ni Vingunguti, Buguruni, Ilala, Kigogo, Magomeni (Kanisa  Katoliki), Kinondoni, Morocco, Makumbusho, Bamaga, ITV, Mwenge kuelekea Hospitali ya Lugalo.

“Mkoa wa Dar es Salaam kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama vya mkoa likiwamo Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, tumejipanga kuimarisha usalama katika maeneo yote ambako mwili wa mpendwa wetu, Dk. Mengi utapita,” amesema Makonda na kuongeza;

“Alifafanua kuwa, siku ya kwanza ni leo ambayo mwili utaletwa, siku ya Jumanne ambayo utaagwa katika viwanja vya Karimjee na siku ya Jumatano utakaposafirishwa kuelekea Machame wilayani Hai, Kilimanjaro kwa maziko siku ya Alhamisi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wami Ruvu hawana deni la Rais Samia katika kutunza vyanzo vya maji

Spread the love  BODI ya Maji Bonde la Wami Ruvu, imeendelea kuchua...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde aibana kampuni kutimiza masharti ya mkataba

Spread the loveWaziri wa Madini, Anthony Mavunde ameitaka Kampuni ya Xin Tai...

Habari Mchanganyiko

Dk. Jafo aipongeza Oryx kumuunga mkono Samia

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Rais, Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Mvungi aendesha kikao kazi cha wataalam wa Regrow

Spread the love  MKURUGENZI wa Idara Sera na Mipango Wizara ya Maliasili...

error: Content is protected !!