Thursday , 28 March 2024
Home Habari Mchanganyiko Buguruni, Ilala, Kinondoni, Mwenge kushuhudia mwili wa Dk. Mengi
Habari MchanganyikoTangulizi

Buguruni, Ilala, Kinondoni, Mwenge kushuhudia mwili wa Dk. Mengi

Spread the love

MWILI wa Dk. Reginald Abraham Mengi, aliyekuwa Mwenyekiti Mtendaji wa Kampuni zilizo chini ya IPP Group, unatarajiwa kuletwa leo saa 8:30 mchana. Anaripoti Bupe Mwakiteleko … (endelea).

Usalama umeimarishwa katika sehemu mbalimbali, hususan maeneo mwili huo utapitishwa baada ya kufikishwa kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Mwalim Julius Nyerere, jijini Dar es Salaam kutoka Dubai, Falme za Kiarabu.

Paul Makonda, Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam amezungumza na wananchi na kueleza barabara ambayo mwili huo utapitishwa pale utapoanza safari kutoka JNIA saa 9:45.

Barabara hizo ni Vingunguti, Buguruni, Ilala, Kigogo, Magomeni (Kanisa  Katoliki), Kinondoni, Morocco, Makumbusho, Bamaga, ITV, Mwenge kuelekea Hospitali ya Lugalo.

“Mkoa wa Dar es Salaam kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi na usalama vya mkoa likiwamo Jeshi la Polisi Kikosi cha Usalama Barabarani, tumejipanga kuimarisha usalama katika maeneo yote ambako mwili wa mpendwa wetu, Dk. Mengi utapita,” amesema Makonda na kuongeza;

“Alifafanua kuwa, siku ya kwanza ni leo ambayo mwili utaletwa, siku ya Jumanne ambayo utaagwa katika viwanja vya Karimjee na siku ya Jumatano utakaposafirishwa kuelekea Machame wilayani Hai, Kilimanjaro kwa maziko siku ya Alhamisi.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wafanyabiashara, wawekezaji China waridhia kuwekeza bil. 800 katika sekta 5 nchini

Spread the loveUJUMBE wa wafanyabiashara na wawekezaji wakubwa kutoka Jimbo la Changzhou...

Habari Mchanganyiko

Bil. 4.42 kumaliza uhaba maji kata 2 Musoma Vijijini

Spread the loveWANANCHI wa kata za Busambara na Kiriba, Jimbo la Musoma...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Soko nepi za watoto lashuka, watu wazima lapaa

Spread the loveKiwanda cha kutengeneza nepi cha Japan kimetangaza kuwa kitaacha kutengeneza...

Habari Mchanganyiko

NMB yafuturisha Dar, Majaliwa azitaka Serikali za Mitaa, Taasisi zijifunze kwao

Spread the loveBENKI ya NMB imewafuturisha wateja wake walio kwenye Mfungo wa...

error: Content is protected !!