Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Chuo cha Diplomasia kimenufaisha 3,421
Habari za Siasa

Chuo cha Diplomasia kimenufaisha 3,421

Spread the love

JUMLA ya wanachuo 3,421 wamehitimu masomo yao katika Chuo cha Diplomasia tangu kuanzishwa kwake mwaka 1978. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 23 Aprili 2019 na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrka Mashariki, Damas Ndumbaro wakati akijibu swali la Mbunge wa Malindi, Ally Salehe Ally (CUF).

Katika swali lake Salehe alitaka kujua Chuo Cha Diplomasia kimetoa wahitimu wangapi tangu kuanzishwa kwake mwaka 1978?

Ndumbaro amesema, wahitimu wa ngazi ya Shahada ni 72, Stashahada  ya Uzamili katika Menejimmenti ya Mahusiano ya kimataifa  ni 503, Shahada uzamili katika Diplomasia ya Uchumi ni 341, Stashahada ya kawaida 2084, ngazi ya cheti ni 347 ni wa mafunzo maalum ya maafisa waandamizi wa Mambo ya Nje.

Amesema, katika idadi hiyo ya wahitimu katika Chuo cha Diplomasia wanawake 1,060 na wanaume 2,361.

Naibu huyo amesema, wanafunzi hao walitoka nchi mbalimbali ikiwemo Afrika Kusini, Algeria, Angola, Butswana, Burundi, Jamhuri ya Kongo, Guinea, Kenya. Comoro, Libya, Malawi na Msumbiji.

Nchi zingine ni pamoja na Namibia, Palestina, Rwanda, Sudan, Zambia, Zimbabwe pamoja na hapa nchini.

Amesema kuwa, tangu kuanzishwa kwa chuo hicho mpaka sasa, wanachuo 500 kutoka Tanzania wamehitimu na kufanya kazi katika maneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Na kwamba, kutokana na umuhimu wa lugha za kufundishia, chuo kwa sasa inafundisha kwa kutumia ya lugha mbalimbali za kigeni katika kufundishia.

Ametaja lugha hizo kuwa ni pamoja na Kifaransa, Kihispania, Kingerreza, Kikorea na Kireno.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!