Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Chuo cha Diplomasia kimenufaisha 3,421
Habari za Siasa

Chuo cha Diplomasia kimenufaisha 3,421

Spread the love

JUMLA ya wanachuo 3,421 wamehitimu masomo yao katika Chuo cha Diplomasia tangu kuanzishwa kwake mwaka 1978. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma … (endelea).

Taarifa hiyo imetolewa leo tarehe 23 Aprili 2019 na Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrka Mashariki, Damas Ndumbaro wakati akijibu swali la Mbunge wa Malindi, Ally Salehe Ally (CUF).

Katika swali lake Salehe alitaka kujua Chuo Cha Diplomasia kimetoa wahitimu wangapi tangu kuanzishwa kwake mwaka 1978?

Ndumbaro amesema, wahitimu wa ngazi ya Shahada ni 72, Stashahada  ya Uzamili katika Menejimmenti ya Mahusiano ya kimataifa  ni 503, Shahada uzamili katika Diplomasia ya Uchumi ni 341, Stashahada ya kawaida 2084, ngazi ya cheti ni 347 ni wa mafunzo maalum ya maafisa waandamizi wa Mambo ya Nje.

Amesema, katika idadi hiyo ya wahitimu katika Chuo cha Diplomasia wanawake 1,060 na wanaume 2,361.

Naibu huyo amesema, wanafunzi hao walitoka nchi mbalimbali ikiwemo Afrika Kusini, Algeria, Angola, Butswana, Burundi, Jamhuri ya Kongo, Guinea, Kenya. Comoro, Libya, Malawi na Msumbiji.

Nchi zingine ni pamoja na Namibia, Palestina, Rwanda, Sudan, Zambia, Zimbabwe pamoja na hapa nchini.

Amesema kuwa, tangu kuanzishwa kwa chuo hicho mpaka sasa, wanachuo 500 kutoka Tanzania wamehitimu na kufanya kazi katika maneo mbalimbali ndani na nje ya nchi.

Na kwamba, kutokana na umuhimu wa lugha za kufundishia, chuo kwa sasa inafundisha kwa kutumia ya lugha mbalimbali za kigeni katika kufundishia.

Ametaja lugha hizo kuwa ni pamoja na Kifaransa, Kihispania, Kingerreza, Kikorea na Kireno.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!