Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mke wa Robert Kisena kuburuzwa kizimbani
Habari Mchanganyiko

Mke wa Robert Kisena kuburuzwa kizimbani

Nyundo ya Hakimu
Spread the love

TAASISI ya Kuzuia na Kupambana na Rushwa Takukuru inatarajia kumburuza kortini Florencia Mashauri ambaye ni mke wa Robart Kisena, Mkurugenzi wa Kampuni ya Usafisirishaji ya UDART. Anaripoti Faki Sosi … (endelea).

Akizungumza na waandishi wa Habari, Kassin Ephrem, Kaimu Mkurugenzi wa Uchunguzi wa Takukuru amesema Taasisi hiyo inampandisha kizimbani Florencia ambaye ni Mkurugenzi wa Kampuni ya Zenon Oil and Gas  Limited kwa tuhuma za kuhujumu uchumi na utakatishaji fedha.

Amesema kuwa mshitakiwa anakabiliwa na tuhumu ya wizi, kukiuka sheria ya mafuta na utakatishaji wa fedha. Pia anadaiwa kutakatisha kiasi cha Sh. 1.2 bilioni na kuitia hasara ya Sh. 1.2 bilioni kwa kuuza mafuta hewa

Florencia na mume wake Kisena naye ameunganishwa kwenye shauri hilo watakalofunguliwa.

MwanaHALISI Online itaendelea kukujulisha kinachoendelea katika shauri hili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!