Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Njooni mnunue korosho-Serikali
Habari Mchanganyiko

Njooni mnunue korosho-Serikali

Spread the love

WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia taasisi yake ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), imewataka wafanyabiashara, taasisi za umma na binafsi kujitokeza kununua korosho ghafi na zilizobanguliwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa tarehe 6 Aprili 2019 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TanTrade, Theresa Chambo, zoezi la uuzaji wa korosho hizo bado linaendelea.
Taarifa hiyo imewataka watu wenye nia ya kununua korosho ghafi na zilizobanguliwa kuwasilisha maombi ya katika mamlaka ya TanTrade, ikiwemo taarifa za kiasi cha korosho wanazohitaji.

“TanTrade inapenda kuwafahamisha kuwa, zoezi la uuzaji korosho linaendelea. Hivyo wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda, hoteli, maduka ya jumla na rejareja, taasisi za umma na binafsi na wananchi kwa ujumla wenye nia ya kununua korosho wanakaribishwa kuwasilisha mahitaji yao,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!