Saturday , 20 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Njooni mnunue korosho-Serikali
Habari Mchanganyiko

Njooni mnunue korosho-Serikali

Spread the love

WIZARA ya Viwanda na Biashara kupitia taasisi yake ya Mamlaka ya Maendeleo ya Biashara Tanzania (TanTrade), imewataka wafanyabiashara, taasisi za umma na binafsi kujitokeza kununua korosho ghafi na zilizobanguliwa. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa tarehe 6 Aprili 2019 na Mkuu wa Kitengo cha Mawasiliano TanTrade, Theresa Chambo, zoezi la uuzaji wa korosho hizo bado linaendelea.
Taarifa hiyo imewataka watu wenye nia ya kununua korosho ghafi na zilizobanguliwa kuwasilisha maombi ya katika mamlaka ya TanTrade, ikiwemo taarifa za kiasi cha korosho wanazohitaji.

“TanTrade inapenda kuwafahamisha kuwa, zoezi la uuzaji korosho linaendelea. Hivyo wafanyabiashara, wamiliki wa viwanda, hoteli, maduka ya jumla na rejareja, taasisi za umma na binafsi na wananchi kwa ujumla wenye nia ya kununua korosho wanakaribishwa kuwasilisha mahitaji yao,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Wauguzi, madaktari 1000 kugawiwa mitungi ya Oryx Gas

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gas na Taasisi ya Doris Mollel Foundation...

Habari Mchanganyiko

Tanzania yachaguliwa Makamu wa Rais Tume ya Shirika la Hali ya Hewa Duniani

Spread the love  TANZANIA kupitia Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA)...

Habari Mchanganyiko

NEMC yaonya wanaojenga bila tathmini ya mazingira

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC),...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

error: Content is protected !!