Tuesday , 30 May 2023
Home Habari Mchanganyiko Mawakili TLS wamtii Lissu
Habari MchanganyikoTangulizi

Mawakili TLS wamtii Lissu

Spread the love

PENDEKEZO la Tundu Lissu, aliyekuwa Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS) kwamba, Dk. Rugemeleza Nshala anafaa kuwa rais wa chama hicho, limetekelezwa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Wajumbe wa TLS jana tarehe 6 Aprili 2019, wamemchagua Dk. Nshala kuwa rais wa chama hicho kwa mwaka mmoja.

Dk. Nshalla amepokea uongozi huo kutoka kwa rais aliyemaliza muda wake, Fatma Karume ambaye aliyehudumu chama hicho kwa mwaka mmoja.

Kabla ya uchaguzi huo, Lissu aliandika kwenye mtandao wa kijamii kwamba, Dk. Nshalla ndio mtu sahihi baada ya Karume.

Katika uchaguzi uliofanyika jana, Dk. Nshala alipata kura 647 kati ya kura zote 1,227 zilizopigwa.

Uchaguzi huo ulifanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Bahame Nyanduga, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, alitaja wagombea wengine katika nafasi ya urais kwamba, walikuwa John Sekka aliyepata kura 29, Gasper Nicodemus kura 58, Godfrey Wasonga kura 123, Godwin Ngwilimi kura 354.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa Rais mpya wa TLS Dk. Nshala, alisema ataendelea kupigania utawala wa sheria na kutekeleza matakwa ya TLS.

Pia TLS itaendelea kuhakikisha wanachama wake wanapata mafunzo mazuri ya sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wenye ulemavu waiomba MISA-TAN iwajengee uwezo wa uhuru wa kujieleza

Spread the love  TAASISI ya vyombo vya Habari kusini mwa Afrika (MISA-TAN)...

Habari Mchanganyiko

Wanawake wajawazito 2000 Korogwe washiriki Marathon, Mwenyekiti UWT amsifu Jokate

Spread the loveWANAWAKE wajawazito zaidi ya 2000 wilayani Korogwe mkoani Tanga wameshiriki...

Habari Mchanganyiko

Kirigini kuzikwa leo Butiama

Spread the love  MWILI wa aliyekuwa Mbunge wa Musoma Vijijini (1980-1985), Herman...

Habari za SiasaTangulizi

Uamuzi juu ya wakurugenzi kusimamia uchaguzi 13 Juni

Spread the love  MAHAKAMA ya Afrika ya Haki za Binadamu (ACHPR), imepanga...

error: Content is protected !!