Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mawakili TLS wamtii Lissu
Habari MchanganyikoTangulizi

Mawakili TLS wamtii Lissu

Spread the love

PENDEKEZO la Tundu Lissu, aliyekuwa Rais wa Chama cha Mawakili wa Tanganyika (TLS) kwamba, Dk. Rugemeleza Nshala anafaa kuwa rais wa chama hicho, limetekelezwa. Anaripoti Mwandishi Wetu…(endelea).

Wajumbe wa TLS jana tarehe 6 Aprili 2019, wamemchagua Dk. Nshala kuwa rais wa chama hicho kwa mwaka mmoja.

Dk. Nshalla amepokea uongozi huo kutoka kwa rais aliyemaliza muda wake, Fatma Karume ambaye aliyehudumu chama hicho kwa mwaka mmoja.

Kabla ya uchaguzi huo, Lissu aliandika kwenye mtandao wa kijamii kwamba, Dk. Nshalla ndio mtu sahihi baada ya Karume.

Katika uchaguzi uliofanyika jana, Dk. Nshala alipata kura 647 kati ya kura zote 1,227 zilizopigwa.

Uchaguzi huo ulifanyika kwenye Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC).

Bahame Nyanduga, Mwenyekiti wa Kamati ya Uchaguzi, alitaja wagombea wengine katika nafasi ya urais kwamba, walikuwa John Sekka aliyepata kura 29, Gasper Nicodemus kura 58, Godfrey Wasonga kura 123, Godwin Ngwilimi kura 354.

Akizungumza mara baada ya kutangazwa Rais mpya wa TLS Dk. Nshala, alisema ataendelea kupigania utawala wa sheria na kutekeleza matakwa ya TLS.

Pia TLS itaendelea kuhakikisha wanachama wake wanapata mafunzo mazuri ya sheria.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

error: Content is protected !!