Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hatma ya pingamizi za serikali kwa Nassari kesho
Habari za Siasa

Hatma ya pingamizi za serikali kwa Nassari kesho

Joshua Nassari
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma kesho tarehe 29 Machi 2019, itatoa uamuzi wa pingamizi tatu, zilizotolewa na serikali katika kesi ya maombi madogo ya kufungua kesi ya msingi, kutengua uamuzi wa Spika wa Bunge la Jamhuri, kumfutia ubunge wa Joshua Nassari (Chadema), katika Jimbo la Arumeru  Mashariki. Anaripoti Danson Kaijage … (endelea).

Kwa mujibu wa Jaji Latifa Mansoor anayesikiliza kesi hiyo namba 22 ya mwaka 2019, amesema mahakama inatarajiwa kusikilizwa pingamizi za serikali tarehe 29 Machi 2019 ambapo hata hivyo, hakutaja pingamizi hizo.

Amesema, uamuzi huo umekuja baada mahakama kupokea pingamizi ziliyotolewa na upande wa serikali ukiwakilishwa na mawakili wawili ambao ni Alisia Mbuya na Masunga Kawahanda.

Tarehe 20 Machi 2019 mahakama ilitoa siku saba kwa upande wa serikali ambao ni Spika wa Bunge la Jamhuri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupeleka kiapo kinzani cha maombi hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!