Tuesday , 3 October 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Hatma ya pingamizi za serikali kwa Nassari kesho
Habari za Siasa

Hatma ya pingamizi za serikali kwa Nassari kesho

Joshua Nassari
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma kesho tarehe 29 Machi 2019, itatoa uamuzi wa pingamizi tatu, zilizotolewa na serikali katika kesi ya maombi madogo ya kufungua kesi ya msingi, kutengua uamuzi wa Spika wa Bunge la Jamhuri, kumfutia ubunge wa Joshua Nassari (Chadema), katika Jimbo la Arumeru  Mashariki. Anaripoti Danson Kaijage … (endelea).

Kwa mujibu wa Jaji Latifa Mansoor anayesikiliza kesi hiyo namba 22 ya mwaka 2019, amesema mahakama inatarajiwa kusikilizwa pingamizi za serikali tarehe 29 Machi 2019 ambapo hata hivyo, hakutaja pingamizi hizo.

Amesema, uamuzi huo umekuja baada mahakama kupokea pingamizi ziliyotolewa na upande wa serikali ukiwakilishwa na mawakili wawili ambao ni Alisia Mbuya na Masunga Kawahanda.

Tarehe 20 Machi 2019 mahakama ilitoa siku saba kwa upande wa serikali ambao ni Spika wa Bunge la Jamhuri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupeleka kiapo kinzani cha maombi hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Bilioni 6.1 kumaliza tatizo la maji Katoro-Buseresere – Geita

Spread the loveMakamu mwenyekiti wa Umoja wa wanawake CCM, (UWT), Zainab Shomari...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali kupokea ndege ya 14 ya ATCL, safari kuongezeka

Spread the love  SERIKALI ya Tanzania, kesho tarehe 3 Oktoba 2023, inatarajia...

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

error: Content is protected !!