Friday , 19 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Hatma ya pingamizi za serikali kwa Nassari kesho
Habari za Siasa

Hatma ya pingamizi za serikali kwa Nassari kesho

Joshua Nassari
Spread the love

MAHAKAMA Kuu Kanda ya Dodoma kesho tarehe 29 Machi 2019, itatoa uamuzi wa pingamizi tatu, zilizotolewa na serikali katika kesi ya maombi madogo ya kufungua kesi ya msingi, kutengua uamuzi wa Spika wa Bunge la Jamhuri, kumfutia ubunge wa Joshua Nassari (Chadema), katika Jimbo la Arumeru  Mashariki. Anaripoti Danson Kaijage … (endelea).

Kwa mujibu wa Jaji Latifa Mansoor anayesikiliza kesi hiyo namba 22 ya mwaka 2019, amesema mahakama inatarajiwa kusikilizwa pingamizi za serikali tarehe 29 Machi 2019 ambapo hata hivyo, hakutaja pingamizi hizo.

Amesema, uamuzi huo umekuja baada mahakama kupokea pingamizi ziliyotolewa na upande wa serikali ukiwakilishwa na mawakili wawili ambao ni Alisia Mbuya na Masunga Kawahanda.

Tarehe 20 Machi 2019 mahakama ilitoa siku saba kwa upande wa serikali ambao ni Spika wa Bunge la Jamhuri na Mwanasheria Mkuu wa Serikali kupeleka kiapo kinzani cha maombi hayo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Tanzania, Uturuki zanuia kukuza biashara, uwekezaji

Spread the loveSERIKALI za Tanzania na Uturuki zimekubaliana kuendeleza dhamira ya kuimarisha...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza ajira watendaji daftari wapiga kura

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC), imetangaza nafasi...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema yatangaza ruti awamu ya pili maandamano

Spread the love  CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimesema awamu ya...

Habari za Siasa

CCM yamkana mwenyekiti UVCCM aliyetaka wapinzani wapotezwe

Spread the love  CHAMA Cha Mapinduzi (CCM), kimejitenga na kauli ya mwenyekiti...

error: Content is protected !!