Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kuchomwa bendera; CUF yatinga kortini
Habari za Siasa

Kuchomwa bendera; CUF yatinga kortini

Halifa Suleiman Halifa, Katibu Mkuu wa CUF akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam
Spread the love

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimefungua shauri mahakamani visiwani Zanzibar kushitaki watu wanaodaiwa kuchoma bendera zake pia kupaka rangi ya bendera ya Chama cha ACT-Wazalendo katika majengo yao. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Halifa Suleiman Halifa, Katibu Mkuu wa CUF akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam leo tarehe 26 Machi 2019 amesema, kesi hiyo imefunguliwa katika Mahakama Kuu ya Vuga visiwani Zanzibar.

Kiongozi huyo wa CUF ameeleza kuwa, wamefungua kesi hiyo baada ya kukusanya ushahidi wa matukio hiyo, ikiwemo kupata majina ya wanayodaiwa kuhusika kuchoma bendera za CUF kubadili rangi za ofisi ya chama hicho na kupaka rangi na nembo za chama cha ACT-Wazalendo.

“Baada ya hapo tukakubaliana tukusanye ushahidi, yote yaliyofanyika, majina ya waliotumika kufuta rangi za chama chetu, waliopachua bendera zetu na kuchoma moto, ushahidi uhuo tumeukamilisha na kufungua kesi katika Mahakama Kuu ya Vuga,” amesema na kuongeza;

“Sasa sheria itachukua mkondo wake, sasa wasishangae moto wao.  Wanasema ShushaTangaPandishaTanga, itamalizikia matanga.

“Kwa tabia hii ya kudhani mtu ni chama ni hatari chama ni taasisi, walipopachua ofisi ya Kilimahewa watu waliwaambia wasipachue, Salim Bimani alisema hilo ni agizo la Maalim Seif.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

Habari za Siasa

Tume huru ya uchaguzi yatangaza uchaguzi mdogo Jimbo la Kwahani

Spread the love  TUME Huru ya Taifa ya Uchaguzi, imetangaza uchaguzi mdogo...

AfyaHabari za Siasa

Dk. Biteko aagiza utoaji huduma saratani usiwe wa kibaguzi

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

error: Content is protected !!