Friday , 9 June 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Kuchomwa bendera; CUF yatinga kortini
Habari za Siasa

Kuchomwa bendera; CUF yatinga kortini

Halifa Suleiman Halifa, Katibu Mkuu wa CUF akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam
Spread the love

CHAMA cha Wananchi (CUF) kimefungua shauri mahakamani visiwani Zanzibar kushitaki watu wanaodaiwa kuchoma bendera zake pia kupaka rangi ya bendera ya Chama cha ACT-Wazalendo katika majengo yao. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Halifa Suleiman Halifa, Katibu Mkuu wa CUF akizungumza na wanahabari jijini Dar es Salaam leo tarehe 26 Machi 2019 amesema, kesi hiyo imefunguliwa katika Mahakama Kuu ya Vuga visiwani Zanzibar.

Kiongozi huyo wa CUF ameeleza kuwa, wamefungua kesi hiyo baada ya kukusanya ushahidi wa matukio hiyo, ikiwemo kupata majina ya wanayodaiwa kuhusika kuchoma bendera za CUF kubadili rangi za ofisi ya chama hicho na kupaka rangi na nembo za chama cha ACT-Wazalendo.

“Baada ya hapo tukakubaliana tukusanye ushahidi, yote yaliyofanyika, majina ya waliotumika kufuta rangi za chama chetu, waliopachua bendera zetu na kuchoma moto, ushahidi uhuo tumeukamilisha na kufungua kesi katika Mahakama Kuu ya Vuga,” amesema na kuongeza;

“Sasa sheria itachukua mkondo wake, sasa wasishangae moto wao.  Wanasema ShushaTangaPandishaTanga, itamalizikia matanga.

“Kwa tabia hii ya kudhani mtu ni chama ni hatari chama ni taasisi, walipopachua ofisi ya Kilimahewa watu waliwaambia wasipachue, Salim Bimani alisema hilo ni agizo la Maalim Seif.”

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Lussu: Mkataba wa DP bandarini si wa miaka 100

Spread the loveMAKAMU Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, amesema hakuna ukweli wowote...

Habari za SiasaTangulizi

Maulid Mtulia: Kutoka ubunge hadi U-DAS

Spread the love ALIYEKUWA mbunge wa Kinondoni, kupitia vyama vya The Civil...

Habari za Siasa

Lusinde: CCM hatuliachii ng’o jimbo la Moshi Mjini

Spread the loveMJUMBE wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (NEC), Livingston...

Habari za SiasaTangulizi

Serikali ya Mapinduzi Zanzibar: Bakharesa hajavamia shamba letu

Spread the love  IKULU Visiwani Zanzibar, imeeleza kuwa eneo la kiwanda cha...

error: Content is protected !!