Wednesday , 1 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Ruge Mutahaba afariki dunia, Rais Magufuli amlilia
Habari MchanganyikoTangulizi

Ruge Mutahaba afariki dunia, Rais Magufuli amlilia

Spread the love

MKURUGENZI wa Vipindi na Uzalishaji wa Clouds Media Group, Ruge Mutahaba amefariki dunia leo nchini Afrika Kusini alipokuwa akipatiwa matibabu. Anaripoti Khalifa Abdallah … (endelea).

Awali, taarifa za kifo cha Ruge zilianza kujulikana mara baada ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dk. John Magufuli kuandika kupitia ukurasa wake wa mtandao wa twitter kuwa amepata taarifa ya kifo hicho.

“Nimepokea kwa masikitiko taarifa za kifo cha kijana wangu Ruge Mutahaba. Daima nitamkumbuka kwa mchango wake mkubwa ktk tasnia ya habari, burudani, na juhudi za kujenga fikra za maendeleo kwa vijana. Poleni wanafamilia,ndugu,jamaa na marafiki. Mungu amweke mahali pema, Amina,” aliandika Rais Magufuli kupitia ukurasa wake rasmi wa Twitter.

Hadi umauti unamfika, Ruge alikuwa nchini Afrika Kusini akipatiwa matibabu ambapo alikuwa akisumbuliwa na tatizo la Figo, aliugua kwa zaidi ya miezi minne akaanza kupatiwa matibu Dar es Salaam katika hospitali ya Kairuki, akapelekwa India na baadae Afrika Kusini ambapo ndipo umauti ulipomkuta.

MwanaHALISI ONLINE itakujuza zaidi. Pumzika kwa amani Ruge Mutahaba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!