Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Udhaifu vituo vya utafiti wamuinua Sugu bungeni
Habari za Siasa

Udhaifu vituo vya utafiti wamuinua Sugu bungeni

Spread the love

MBUNGE wa Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi (Sugu) kutoka Chadema ameiomba serikali kueleza ni lini itatenga fedha za kutosha kwa ajili ya kufufua vituo vya utafiti kama vile Chuo cha Utafiti kilichopo Uyole, Mbeya. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Akiuliza swali la nyongeza bungeni Mbilinyi amesema kuwa, kwa sasa Chuo cha Uyole kinakabiliwa na miundombinu pamoja na ufinyu wa bajeti.

Amehoji, lini serikali itaweza kuweka mipango ya kuongeza bajeti ili kuweza kufanya chuo hicho kuwa na miundombinu pia kukiongezea bajeti ili kiweze kufanya vizuri zaidi.

Katika swali la msingi la Martin Msua, Mbunge wa Mbinga Vijijini (CCM) aliyetaka kujua ni lini serikali ilifanya utafiti wa gharama za uzalishaji wa kahawa wilayani Mbinga kwa mara ya mwisho.

Akijibu maswali hayo Omar Mgumba, Naibu Waziri wa Kilimo amesema, serikali ilipeleka mswada wa Sheria bungeni na kuunda vituo 16 ambapo kila kituo kitakuwa kikifanya utafiti wa mazao mawili tu.

Mgumba amesema, lengo la kufanya kila kituo kufanya utafiti wa ni kufanya vituo hivyo visiweze kulemewa katika utendaji wao wa kazi.

Akizungumzia suala la kuwezesha kituo kikubwa cha Utafiti cha Uyole amesema, katika bajeti ya mwaka wa fedha 2019/20 watakitengea fedha chuo hicho.

Mgumba amesema kuwa, serikali katika mwaka wa fedha 2015/2016 kupitia taasisi ya Utafiti wa Kahawa Tanzania (TaCRI) imefanya utafiti wa uzalishaji wa kahawa katika wilaya saba;- Mbinga, Mbozi, Tarime,Rombo, Muleba, Karagwe na Buhigwe.

Amesema, utafiti uliofanywa na TaCRI kwa wakulima wa kahawa aina ya Arabca unaonesha gharama za uzalishaji wa aina bora za kahawa zenye ukinzani wa magonjwa Sh. 2.1 Mil kwa heka sawa na wastani wa Sh. 843.4 kwa kilo zenye tija ya wastani wa kilo 2662 kwa hekta.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!