Saturday , 3 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Mkakati wa serikali kwa bodaboda ni huu
Habari Mchanganyiko

Mkakati wa serikali kwa bodaboda ni huu

Anthony Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira.
Spread the love

SERIKALI imeainisha mikakati mitano inayofanya katika kuwajengea uwezo waendesha bodaboda ukiwemo faida za kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo bungeni na Antony Mavunde, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Vijana, Kazi na Ajira wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Lushoto, Shabani Shekilindi (CCM).

Katika swali hilo, mbunge huyo alisema uendeshaji bodaboda ni ajira kama zilivyo ajira nyingine nchini.

Amehoji, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea uwezo vijana hao ili kuifanya kazi yao hiyo iwe rasmi na yenye kutambulika kama kazi nyingine zozote.

Akifafanua Mavunde amesema, mipango hiyo ni pamoja na kutoa mafunzo ya udereva kupitia Jeshi la Polisi kwa waendesha bodaboda na hatimaye kupatiwa leseni za udereva.

Aidha, kama ilivyo vyombo vingine vinavyotoa huduma za usafiridhaji, usalama wa waendesha bodaboda na abiria umeendelea kusimamiwa na kulindwa wanapotekeleza majukumu yao barabarani.

Mwingine ni kuhamasisha uundwaji wa vikundi vya waendesha bodaboda ili hatimaye viweze kuwezeshwa kwa mitaji na mafunzo kupitia mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi na wadaiu wengine.

Aidha, kuwapatia maeneo ya kuegesha bodaboda ya kuyatambua pamoja na kuwapatia vitambulisho.

Pia, kuwapatia waendesha bodaboda mafunzo ya ujasiriamali na hatimaye kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu na kuwaunganisha na taasisi zingine zinazotoa mikopo.

Na kuwa, watapatiwa elimu juu ya faida za kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na kuwaunganisha na mifuko husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Magunia 731 ya bangi yakamatwa, mamia ya hekari yateketezwa Arumeru

Spread the love  MAMIA ya magunia ya madawa ya kulevya aina ya...

Habari MchanganyikoTangulizi

Bosi NIC apandishwa kizimbani, akabiliwa na mashitaka 365

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la Bima la Taifa...

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

error: Content is protected !!