Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mkakati wa serikali kwa bodaboda ni huu
Habari Mchanganyiko

Mkakati wa serikali kwa bodaboda ni huu

Anthony Mavunde, Naibu Waziri Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Kazi, Vijana na Ajira.
Spread the love

SERIKALI imeainisha mikakati mitano inayofanya katika kuwajengea uwezo waendesha bodaboda ukiwemo faida za kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii. Anaripoti Danson Kaijage, Dodoma…(endelea).

Kauli hiyo imetolewa leo bungeni na Antony Mavunde, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Vijana, Kazi na Ajira wakati akijibu swali la msingi la Mbunge wa Lushoto, Shabani Shekilindi (CCM).

Katika swali hilo, mbunge huyo alisema uendeshaji bodaboda ni ajira kama zilivyo ajira nyingine nchini.

Amehoji, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea uwezo vijana hao ili kuifanya kazi yao hiyo iwe rasmi na yenye kutambulika kama kazi nyingine zozote.

Akifafanua Mavunde amesema, mipango hiyo ni pamoja na kutoa mafunzo ya udereva kupitia Jeshi la Polisi kwa waendesha bodaboda na hatimaye kupatiwa leseni za udereva.

Aidha, kama ilivyo vyombo vingine vinavyotoa huduma za usafiridhaji, usalama wa waendesha bodaboda na abiria umeendelea kusimamiwa na kulindwa wanapotekeleza majukumu yao barabarani.

Mwingine ni kuhamasisha uundwaji wa vikundi vya waendesha bodaboda ili hatimaye viweze kuwezeshwa kwa mitaji na mafunzo kupitia mifuko ya uwezeshaji wananchi kiuchumi na wadaiu wengine.

Aidha, kuwapatia maeneo ya kuegesha bodaboda ya kuyatambua pamoja na kuwapatia vitambulisho.

Pia, kuwapatia waendesha bodaboda mafunzo ya ujasiriamali na hatimaye kuwapatia mikopo yenye masharti nafuu na kuwaunganisha na taasisi zingine zinazotoa mikopo.

Na kuwa, watapatiwa elimu juu ya faida za kujiunga na mifuko ya hifadhi ya jamii pamoja na kuwaunganisha na mifuko husika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Wakili: Ukimpa zawadi mwenza marufuku kumpora hata mkiachana

Spread the love  WANANDOA na watu waliko kwenye mahusiano ya kimapenzi, wamekumbushwa...

Habari Mchanganyiko

Majaliwa: Mvua zimesababisha vifo vya watu 155, kuendelea hadi Mei

Spread the love  WAZIRI Mkuu, Kassim Majaliwa amesema mvua kubwa za El-Nino...

Habari Mchanganyiko

Exim Bank yatoa  vitanda kwa shule ya Jeshi la Polisi Moshi

Spread the love  BENKI ya Exim imekabidhii  seti ya vitanda kwa Shule...

Habari Mchanganyiko

NBC yakabidhi vitanda Shule ya Polisi Moshi

Spread the loveBenki ya NBC imekabidhi msaada wa vitanda 28 kwa Shule...

error: Content is protected !!