Wednesday , 1 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Prof. Lipumba amgeuka Jaji Mutungi
Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba amgeuka Jaji Mutungi

Spread the love

MTAFARUKU mkubwa umeibuka ndani ya Kamati ya Bunge ya Katiba na Sheria, kufuatia mwenyekiti wa kamati hiyo, Mohammed Nchengerwa, kuamuru pande mbili zinazopingana ndani ya Chama cha Wananchi (CUF), kugawana muda wa kutoa maoni ndani ya kamati hiyo. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Taarifa kutoka ndani ya Kamati ya Katiba na Sheria zinaeleza kuwa mara baada ya Nchengerwa kuelekeza kuwa kila upande kati ya Prof. Ibrahim Lipumba, mwenyekiti anayetambuliwa na msajili wa vyama na Maalim Seif Shariff Hamad, katibu mkuu wa chama hicho anayetambuliwa na wanachama wa chama hicho.

Kwa mujibu wa taarifa hizo, mgogoro huo ulipamba moto kufuatia baadhi ya wajumbe wa kamati hiyo, kushinikiza mwenyekiti kutoa dakika 30 kwa kila upande. Nchengerwa aligomea pendekezo hilo.

Akizungumza ndani ya kamati ya katiba na sheria, Prof. Lipumba alisema, msajili wa vyama hana nguvu ya kukikaba Chama Cha Mapinduzi (CCM), kuliko anavyoweza kuvikaba vyama vya upinzani.

Alisema,“…huyu msajili wa vyama vya siasa, ni mteule wa rais ambaye ni mwenyekiti wa chama kilichoko madarakani. Hivyo kwa vyovyote vile, anaweza kuvibana vyama vya upinzani kuliko anavyoweza kukishughulikia chama tawala.”

Alipoulizwa kuhusu nafasi ya msajili wa vyama vya siasa, katika kutatua migogoro ya ndani ya vyama hivyo, Prof. Lipumba alisema, “uwezo huo ni mdogo sana.” Alisema, migogoro ndani ya vyama, inapaswa kutatuliwa ndani ya vyama vyenyewe.

Aidha, Prof. Lipumba alidai kuwa vifungu vinavyotoa mamlaka kwa msajili wa vyama kutoa taarifa kuhusu mafunzo ya ndani ya vyama hivyo, haviwezi kutekelezeka kwa kuwa ofisi hiyo haina uwezo wa kufanya kazi hiyo.

Naye Joram Bashange, kaimu katibu mkuu wa CUF Tanzania Bara, ameiambia kamati ya katiba na sheria, kwamba muswaada uliopo ndani ya Bunge, ni mgumu kwa vyama hivyo kufanya kazi zake kama inavyotakiwa.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

Habari za Siasa

Mavunde aomba bilioni 231.9 bajeti wizara ya madini

Spread the loveWAZIRI wa Madini, Anthony Mavunde leo Jumanne amewasilisha hotuba ya...

Habari za SiasaTangulizi

Lissu amjibu Fatma Karume kuhusu Rais Samia

Spread the love  MAKAMU Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema)...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Slaa: Watanzania iungeni mkono Chadema uchaguzi 2025

Spread the loveMWANASIASA mkongwe nchini Tanzania, Dk. Wilbroad Slaa, amewataka watanzania wakiunge...

error: Content is protected !!