Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Tanzania wasaka soko la korosho Algeria
Habari MchanganyikoTangulizi

Tanzania wasaka soko la korosho Algeria

Naibu Waziri wa Mambo ya Nje Dk. Damas Ndumbaro amekutana na kufanya mazungumzo na Balozi wa Algeria, Saad Belabed
Spread the love

SERIKALI imefanya mazungumzo na Algeria kuhusu masuala ya diplomasia ya kiuchumi, ambapo nchi hiyo imeonyesha nia ya kutaka kununua korosho za Tanzania. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Akizungumza na vyombo vya habari leo tarehe 8 Januari 2019, Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dk. Damas Ndumbaro amesema Tanzania na Algeria ziko kwenye mazungumzo ya mwisho ambayo yatapelekea kukamilisha zoezi hilo la biashara ya korosho.

Dkt. Ndumbaro ameeleza kuwa, soko hilo limepatikana baada ya kuzungumza na Balozi wa Algeria nchini Tanzania, na kwamba kutokana na mazungumzo hayo, ni wazi kuwa korosho zinazolimwa hapa nchini zitapata soko Algeria.

“Nimekutana na mabalozi wa wawili , balozi wa kwanza ni wa Algeria nchini Tanzania ambaye tumefanya kikao kizuri sana kujadili masuala yanayohusu diplomasia ya kiuchumi, katika mkutano wetu tumeweza kujadili kuhusu suala la soko la korosho, wameonyesha nia ya kutaka kununua korosho. Hivyo tumefanya mazungumzo ya awali, kutokana na mazungumzo ya awali ni wazi sasa korosho ya Tanzania itapata soko Algeria,” amesema na kuongeza Dk. Ndumbaro.

“Na tayari tumewasiliana na wenzetu wa wizara ya viwanda na biashara, wamelipokea suala hili kwa mikono miwili na sasa tunaenda kwenye mazungumzo ya mwisho ambayo yatapelekea kukamilisha zoezi hilo la biashara ya korosho kati ya Tanzania na Algeria.”

Katika hatua nyingine, Dk. Ndumbaro amesema Serikali ya Awamu ya Tano inayoongozwa na Rais John Magufuli inafanya kila juhudi kuhakikisha inawakomboa kiuchumi wakulima wa Tanzania na hasa katika kutafuta masoko ya mazao nje ya nchi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

Habari Mchanganyiko

Chongolo aonya viongozi vijiji kutouza NIDA kwa wageni

Spread the loveMKUU wa Mkoa wa Songwe, Daniel Chongolo amewaonya viongozi wa...

Habari Mchanganyiko

TUCTA, OSHA wataka kampuni za madini kuiga ubunifu wa GGML

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA) pamoja na Wakala...

error: Content is protected !!