Tuesday , 23 April 2024
Home Kitengo Habari Kimataifa Rais wa Benki ya Dunia ajiuzulu ghafla
Kimataifa

Rais wa Benki ya Dunia ajiuzulu ghafla

Rais wa Benki ya Dunia (W.B), Jim Yong Kim
Spread the love

RAIS wa Benki ya Dunia (W.B), Jim Yong Kim aliyehudumu katika wadhifa huo tangu mwaka 2012 hadi mwanzoni mwa mwaka huu, amejiuzulu ghafla. Inaripoti Mitandao ya Kimataifa … (endelea).

Kim ambaye alitakiwa kumaliza muda wake mwishoni mwa mwaka 2021, ametangaza uamuzi wake wa kujiuzulu jana Jumatatu tarehe 7 Januari 2019.

Katika tamko lake hakueleza sababu za kujiuzulu, zaidi ya kusema kwamba kazi ya W.B ni ya muhimu katika kipindi hiki kuliko kipindi kingine kutokana na ongezeko la masikini, matatizo ya mabadiliko ya hali ya hewa, njaa na wakimbizi.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na W.B kwa vyombo vya habari inaeleza kuwa, Kim atajiunga na shughuli za uimarishaji uwekezaji wa miundombinu katika nchi zinazoendelea pamoja na kurejea katika Bodi ya Shirika la Afya, aliyoianzisha miongo mitatu iliyopita.

Tangu benki hiyo ilipoanzishwa mwishoni mwa vita kuu ya pili ya dunia, W.B imekuwa ikiongozwa na Wamarekani, ambapo viongozi wake walikuwa wanachaguliwa na rais wa Marekani.

Hivyo, Rais wa sasa wa taifa hilo, Donald Trump anatarajiwa kuteua mrithi wa Kim.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

KimataifaTangulizi

Mkuu wa majeshi Kenya afariki, Ruto atangaza maombolezo

Spread the loveRais wa Kenya, William Ruto ametangaza maombezo ya siku tatu...

Kimataifa

Majaji kuamua hatima ya Zuma leo

Spread the loveMajaji nchini Afrika Kusini leo Jumanne wataamua ikiwa rais wa...

Habari za SiasaKimataifa

Spika Afrika Kusini ajiuzulu kwa tuhuma za rushwa

Spread the loveSpika wa Bunge la Afrika Kusini, Nosiviwe Mapisa-Nqakula ametangaza kujiuzulu...

Habari MchanganyikoKimataifa

Tetemeko la ardhi laua 7, lajeruhi 800 Taiwan

Spread the loveWatu wapatao saba wamefariki dunia na wengine zaidi ya 800...

error: Content is protected !!