Saturday , 27 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa CAG kufanya ukaguzi maalum kwenye miradi ya maji
Habari za Siasa

CAG kufanya ukaguzi maalum kwenye miradi ya maji

Spread the love

SERIKALI imeshauriwa kumruhusu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad kufanya ukaguzi maalum kwenye miradi ya maji kutokana na uwepo wa madai ya miradi hiyo kutekelezwa chini ya kiwango. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Ombi hilo limetolewa leo tarehe 16 Novemba 2018 bungeni jijini Dodoma, na Mbunge Viti Maalum, Conchesta Rwamlaza akisema kwamba kuna malalamiko mengi ya miradi ya maji kutekelezwa chini ya kiwango, na kushauri CAG kufanya ukaguzi maalum ili kujua utekelezwaji wa miradi hiyo na kiasi cha fedha kilichotumika katika utekelezwaji wake.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Maji, Juma Aweso amesema haina haja ya kuagiza ukaguzi maalum wa CAG kwa kuwa wizara imeunda timu maalum ya wataalam kwa ajili ya kukagua miradi ya maji hasa maeneo ya vijijini.

“CAG amekuwa akifanya ukaguzi kila mwaka, ukaguzi wa miradi kuhusu ufanisi na utaalamu hufanyika kila mwaka, CAG ameshafanya ukaguzi kwenye usimamizi wa uchimbaji wa visima vya maji na miradi iliyokamilkia, taarifa ya ukaguzi ilikaguliwa na kuwasilishwa bungeni, ukaguzi wa ufanisi na wa kitaalamu , serikali haina haja ya kuagiza ukaguzi maalum, wizara iliunda timu ya wataalam maalum kukagua miradi ya maji vijijini,”amesema Aweso.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Sauti ya Watanzania waeleza sababu za kuiunga mkono Chadema

Spread the love  KIKUNDI kinachojipambanua katika kupigania rasilimali na uhuru wa nchi,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari za Siasa

ACT: Waongoza watalii wapate maslahi yao inavyostahili

Spread the loveCHAMA cha ACT-Wazalendo kimeitaka serikali kuhakikisha inasimamia maslahi stahiki ya...

Habari za SiasaTangulizi

Prof. Lipumba ajitosa kuviunganisha vyama vya siasa Burundi

Spread the love  MWENYEKITI wa Kituo Cha Demokrasia Tanzania (TCD), Prof. Ibrahim...

error: Content is protected !!