Friday , 29 September 2023
Home Gazeti Habari za Siasa CAG kufanya ukaguzi maalum kwenye miradi ya maji
Habari za Siasa

CAG kufanya ukaguzi maalum kwenye miradi ya maji

Spread the love

SERIKALI imeshauriwa kumruhusu Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG), Profesa Mussa Assad kufanya ukaguzi maalum kwenye miradi ya maji kutokana na uwepo wa madai ya miradi hiyo kutekelezwa chini ya kiwango. Anaripoti Regina Mkonde … (endelea).

Ombi hilo limetolewa leo tarehe 16 Novemba 2018 bungeni jijini Dodoma, na Mbunge Viti Maalum, Conchesta Rwamlaza akisema kwamba kuna malalamiko mengi ya miradi ya maji kutekelezwa chini ya kiwango, na kushauri CAG kufanya ukaguzi maalum ili kujua utekelezwaji wa miradi hiyo na kiasi cha fedha kilichotumika katika utekelezwaji wake.

Akijibu swali hilo, Naibu Waziri wa Maji, Juma Aweso amesema haina haja ya kuagiza ukaguzi maalum wa CAG kwa kuwa wizara imeunda timu maalum ya wataalam kwa ajili ya kukagua miradi ya maji hasa maeneo ya vijijini.

“CAG amekuwa akifanya ukaguzi kila mwaka, ukaguzi wa miradi kuhusu ufanisi na utaalamu hufanyika kila mwaka, CAG ameshafanya ukaguzi kwenye usimamizi wa uchimbaji wa visima vya maji na miradi iliyokamilkia, taarifa ya ukaguzi ilikaguliwa na kuwasilishwa bungeni, ukaguzi wa ufanisi na wa kitaalamu , serikali haina haja ya kuagiza ukaguzi maalum, wizara iliunda timu ya wataalam maalum kukagua miradi ya maji vijijini,”amesema Aweso.

 

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yawaangukia viongozi wa dini

Spread the loveSERIKALI imewaomba viongozi wa dini, waendelee kuelimisha wananchi kudumisha amani...

Habari za Siasa

Azzim Dewji aitaka Serikali iwanyooshe mafisadi

Spread the loveMFANYABIASHARA maarufu nchini, Azzim Dewji, ameitaka Serikali iwachukulie hatua wezi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari za Siasa

Mgongano wa kimasilahi wamhamisha Chande TTCL

Spread the love  ALIYEKUWA Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO),...

error: Content is protected !!