Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo Kocha Simba ang’aka Uwanja Mkwakwani
Michezo

Kocha Simba ang’aka Uwanja Mkwakwani

Patrick Aussems, Kocha Mkuu wa Simba
Spread the love

KOCHA Mkuu wa Simba, Patric Aussems ameonekana kutorizishwa na nyasi za uwanja wa Mkwakwani uliopo mkoani Tanga mara baada ya kufanya mazoezi ya siku mbili na kikosi chake ambacho kitaivaa JKT Tanzania  ambao watakuwa wenyeji wachezo huo wa Ligi Kuu Tanzania Bara. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Aussems amebainisha hayo kupitia ukurasa wake unaopatikana kwenye mtandao wa kijamii wa Twitter mara baada tu yakuwasili na kikosi chake mkoani humo kwa ajili ya kusaka alama tatu ambazo zitamsaidia katika kutetea ubingwa wa ligi hiyo.

“Hali ya Uwanja Tanga kwa mchezo wetu wa kesho dhidi ya JKT, kivipi inawezekana? Maendeleo ya mpira katika nchi yatawezekana kama kutakuwa na miundombinu mizuri.”

Simba ambao toka ligi ianze msimu huu wamekuwa hawana rekodi nzuri wanapokuwa katika michezo ya ugenini, katika michezo mitatu Simba iliyocheza ugenini imefanikiwa kushinda mmoja, sare mmoja na kupoteza mmoja dhidi ya Mbao FC katika Uwanja wa CCM Kirumba.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!