Friday , 29 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Magari ya Serikali yagongana, saba wafariki
Habari Mchanganyiko

Magari ya Serikali yagongana, saba wafariki

Spread the love

WATUMISHI saba wamefariki dunia wakati watatu wakijeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari la Ofisi ya Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), iliyotokea usiku wa kuamkia leo tarehe 3 Novemba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza kuhusu ajali hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Murotto amesema chanzo cha ajali hiyo iliyotokea wilayani Kongwa, ni kuegeshwa kwa roli aina ya DAF yenye namba za usajili T161 CBB/T152 CBB, barabarani na kupelekea gari ya ofisi ya CAG aina ya Toyota Land Cruiser (STL 6250) kuigonga kwa nyuma .

Kamanda Murotto ameeleza kuwa, baada ya gari hilo kuligonga roli kwa nyuma, iligongana uso kwa uso na gari lingine aina ya Toyota Land Cruiser ya PSSSF. Gari ya CAG ilikuwa ianendeshwa na Dickson Kitanda (42) ikitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam, na gari la PSSSF lilikuwa linaendeshwa na Peter Elleson Masamu (35).

Gari la ofisi ya CAG lilikuwa na abiria saba na gari la PSSSF lilikuwa na abiria watatu.

Kamanda Murotto amesema miili ya marehemu imepelekwa kuhifadhiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Kongwa na majeruhi wamelazwa hos[pitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Stamico yafungua fursa za kiuchumi kwa makundi maalumu

Spread the loveSHIRIKA la Madini la Taifa (STAMICO) limemwaga neema kwa watu...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Maabara ya bilioni 5 upimaji madini yazinduliwa Geita, inapima kwa mionzi

Spread the loveZaidi ya Sh bilioni tano zimewekezwa katika kampuni ya MSALABS...

ElimuHabari Mchanganyiko

Wanafunzi Nyamkumbu wanolewa na GGML kuhusu taaluma ya madini

Spread the loveZAIDI ya Wanafunzi 50 kutoka Shule ya Sekondari ya Wasichana...

Habari Mchanganyiko

Makamba: China ni ya mfani kwa kupunguza umaskini

Spread the loveWAZIRI wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, January...

error: Content is protected !!