Thursday , 18 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Magari ya Serikali yagongana, saba wafariki
Habari Mchanganyiko

Magari ya Serikali yagongana, saba wafariki

Spread the love

WATUMISHI saba wamefariki dunia wakati watatu wakijeruhiwa katika ajali iliyohusisha gari la Ofisi ya Mdhibiti Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) na Mfuko wa Hifadhi ya Jamii kwa Watumishi wa Umma (PSSSF), iliyotokea usiku wa kuamkia leo tarehe 3 Novemba 2018. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Akizungumza kuhusu ajali hiyo, Kamanda wa Polisi mkoani Dodoma, Gilles Murotto amesema chanzo cha ajali hiyo iliyotokea wilayani Kongwa, ni kuegeshwa kwa roli aina ya DAF yenye namba za usajili T161 CBB/T152 CBB, barabarani na kupelekea gari ya ofisi ya CAG aina ya Toyota Land Cruiser (STL 6250) kuigonga kwa nyuma .

Kamanda Murotto ameeleza kuwa, baada ya gari hilo kuligonga roli kwa nyuma, iligongana uso kwa uso na gari lingine aina ya Toyota Land Cruiser ya PSSSF. Gari ya CAG ilikuwa ianendeshwa na Dickson Kitanda (42) ikitokea Dodoma kuelekea Dar es Salaam, na gari la PSSSF lilikuwa linaendeshwa na Peter Elleson Masamu (35).

Gari la ofisi ya CAG lilikuwa na abiria saba na gari la PSSSF lilikuwa na abiria watatu.

Kamanda Murotto amesema miili ya marehemu imepelekwa kuhifadhiwa katika chumba cha maiti cha Hospitali ya Kongwa na majeruhi wamelazwa hos[pitali ya rufaa ya mkoa wa Dodoma.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

Habari Mchanganyiko

Serikali yatoa ajira watumishi 46,000, yatangaza utaratibu mpya kuajiri

Spread the loveSERIKALI imetangaza nafasi za ajira za watumishi wa umma 46,000...

error: Content is protected !!