Thursday , 2 May 2024
Home Kitengo Michezo FIFA yamfungia maisha kiongozi CAF
Michezo

FIFA yamfungia maisha kiongozi CAF

Kwesi Nyantakyi
Spread the love

SHIRIKISHO la Mpiwa wa Miguu Duniani (FIFA) limemfungia maisha kujihusisha na masuala ya soka aliyekuwa Rais wa Shirikisho la Soka nchini Ghana (GFA), Kwesi Nyantakyi baada ya kukutwa na hatia ya kupokea rushwa ya kiasi cha dola 65,000 kutoka kwa mwandishi wa shirika la habari la England, Anas Aremeyaw. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endeleaa). 

Shirikisho hilo lilifanya uchunguzi kwa kina kujua kama kweli alihusika kupokea kiasi hicho cha pesa kutoka kwa mwandishi huyo ambaye alitumwa kwa kazi maalum ya kupima uaminifu wa rais huyo na baadaye kumkuta na hatia na kuchukua maamuzi hayo.

Baada ya tuhuma hizo Nyantakyi ambaye aliwahi kuwa Makamu wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) na mjumbe wa halmashauli kuu ya Fifa alijiuzuru nafasi yake ya urais GFA mwezi juni na kujivua nyadhifa zake zote za CAF na FIFA ingawa hakuna mahari alipo kubali kuwa alipokea kiasi hicho cha fedha.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!