Friday , 26 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ugonjwa wa moyo wampeleka Mbowe nje ya nchi
Habari za Siasa

Ugonjwa wa moyo wampeleka Mbowe nje ya nchi

Freeman Mbowe, Mwenyekiti wa Chadema
Spread the love

MWENYEKITI wa Chadema Taifa, Freeman Mbowe ameshindwa kufika katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu, kutokana na kuwa nje ya nchi kwa ajili ya matibabu ya ugonjwa wa moyo na shinikizo la damu. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Mdhamini wa Mbowe, Grayson Celestine ameieleza mahakama akidai kuwa, aliwasiliana na mke wa Mbowe jana ambaye alimueleza kwamba, Mbowe amesafirishwa kwa dharula nje ya nchi na familia yake, kwa ajili ya kupatiwa matibabu.

Kuali hiyo ilitolewa baada ya Mbowe ambaye ni mshtakiwa wa kwanza katika kesi ya jinai Na. 112/2018, kushindwa kupanda kizimbani huku washtakiwa wengine wanane wakipanda kizimbani katika mahakama hiyo.

Kutokana na Mbowe kutohudhuria mahakamani, Wakili Mkuu wa Serikali, Faraja Nchimbi aliiomba mahakama kutoa amri, Mbowe akamatwe ili aeleze kwa nini dhamana aliyopewa isifutwe kutokana na kushindwa kufika mahakamani.

Kufuatia hoja hizo, Hakimu Wilbard Mashauri alihoji kama Mbowe ana uthibitisho kwamba alisafiri nje ya nchi kwa ajili ya matibabu, na kujibiwa na Celestine akidai kuwa mtuhumiwa huyo akirejea nchini atawasilisha nyaraka za safari na matibabu.

Hakimu Mashauri amesema endapo Mbowe hatopeleka uthibitisho mahakani hapo, atatoa amri ya kumkamata ili ajieleze kwa nini asifutiwe dhamana kwa kukiuka masharti ya dhamana aliyopewa na mahakama.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Prof. Muhongo akomalia matumizi nishati jadidifu kuondoa uhaba wa umeme

Spread the love  MBUNGE wa Musoma Vijijini (CCM), Profesa Sospeter Muhongo, ameendelea...

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

error: Content is protected !!