Friday , 3 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Raia wa kigeni wanaswa wakitorosha dola 70,000
Habari MchanganyikoTangulizi

Raia wa kigeni wanaswa wakitorosha dola 70,000

Spread the love

RAIA wawili wa kigeni, Nada Zaelnoon Ahamed (38) na Mohamed Belal (31), wanashikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kukutwa na kiasi cha Dola za Kimarekani 70,000 (Sh. 190 milioni), wakitaka kuzisafirisha kwenda nje ya nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Nada Ahamed (38), ni raia kutoka Sudan Kusini na Mohamed Belal (31) anatokea nchini Syria. Wote wawili wamekamatwa kwenye kiwanja cha Ndege cha Kimataifa (JNIA).

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Baranabas Mwakalukwa amesema, watuhumiwa hao wamekamatwa kufuatia kushindwa kutoa taarifa juu ya fedha walizokuwa nazo.

Amesema, kitendo cha kutotoa taarifa ya fedha kwa wasafiri wanaotaka kusafirisha kiasi kikubwa cha fedha, ni kinyume na Sheria ya Utakatishaji Fedha ya mwaka 2006 iliyofanyiwa marekebisho 2012.

Kwa mujibu wa Mwakalukwa, Nada alikuwa anaelekea Nairobi nchini Kenya. Alikuwa anatumia ndege ya Shirika la Kenya Airways na Mohamed alikuwa akielekea nchini Syria. Alikuwa anatumia ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.

Amesema, Nada ndiye aliyekuwa wa kwanza kukamatwa na fedha hizo, ambapo alikutwa na dola 60,000 na paundi za Sudani 3,410 na kwamba baada ya kubanwa alimtaja mshirika wake Belal aliyenaswa na dola 10,000 (elfu kumi).

Kamanda Mwakalukwa amesema, watuhumiwa hao wamezuiwa na kwamba hawawezi kuendelea na safari zao kwa ajili ya kupisha uchunguzi ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Kufuatia tukio hilo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Richard Mayongela, ametoa wito kwa wasafiri, wadau na watumishi wa mamlaka hiyo na vyombo vya dola kutoa taarifa za vitendo vya kihalifu ili mamlaka stahiki zichukue hatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kumshtaki Rais Samia

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimetishia kumfungulia kesi ya...

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB yang’ara maonesho OSHA

Spread the loveBenki ya NMB imebeba tuzo ya kampuni bora kwenye sekta...

Habari MchanganyikoKimataifa

Ruto amteua Kahariri kuwa mkuu wa majeshi

Spread the loveRAIS wa Kenya, William Ruto, amemteua Jenerali Charles Muriu Kahariri,...

error: Content is protected !!