Friday , 2 June 2023
Home Habari Mchanganyiko Raia wa kigeni wanaswa wakitorosha dola 70,000
Habari MchanganyikoTangulizi

Raia wa kigeni wanaswa wakitorosha dola 70,000

Spread the love

RAIA wawili wa kigeni, Nada Zaelnoon Ahamed (38) na Mohamed Belal (31), wanashikiliwa na Jeshi la Polisi baada ya kukutwa na kiasi cha Dola za Kimarekani 70,000 (Sh. 190 milioni), wakitaka kuzisafirisha kwenda nje ya nchi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Nada Ahamed (38), ni raia kutoka Sudan Kusini na Mohamed Belal (31) anatokea nchini Syria. Wote wawili wamekamatwa kwenye kiwanja cha Ndege cha Kimataifa (JNIA).

Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini, Baranabas Mwakalukwa amesema, watuhumiwa hao wamekamatwa kufuatia kushindwa kutoa taarifa juu ya fedha walizokuwa nazo.

Amesema, kitendo cha kutotoa taarifa ya fedha kwa wasafiri wanaotaka kusafirisha kiasi kikubwa cha fedha, ni kinyume na Sheria ya Utakatishaji Fedha ya mwaka 2006 iliyofanyiwa marekebisho 2012.

Kwa mujibu wa Mwakalukwa, Nada alikuwa anaelekea Nairobi nchini Kenya. Alikuwa anatumia ndege ya Shirika la Kenya Airways na Mohamed alikuwa akielekea nchini Syria. Alikuwa anatumia ndege ya Shirika la Ndege la Ethiopia.

Amesema, Nada ndiye aliyekuwa wa kwanza kukamatwa na fedha hizo, ambapo alikutwa na dola 60,000 na paundi za Sudani 3,410 na kwamba baada ya kubanwa alimtaja mshirika wake Belal aliyenaswa na dola 10,000 (elfu kumi).

Kamanda Mwakalukwa amesema, watuhumiwa hao wamezuiwa na kwamba hawawezi kuendelea na safari zao kwa ajili ya kupisha uchunguzi ili hatua za kisheria zichukuliwe dhidi yao.

Kufuatia tukio hilo, Mkurugenzi wa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege Tanzania (TAA), Richard Mayongela, ametoa wito kwa wasafiri, wadau na watumishi wa mamlaka hiyo na vyombo vya dola kutoa taarifa za vitendo vya kihalifu ili mamlaka stahiki zichukue hatua.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari Mchanganyiko

Serikali yakabidhi eneo la mahakama ya Afrika ya haki za binadamu

Spread the loveSerikali kupitia Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa...

Habari Mchanganyiko

Udhamini wa NMB mikutano ya ALAT wafikia 1.2 bilioni

Spread the loveBENKI ya NMB imeendelea kufanya kazi kwa karibu na Asasi...

Habari Mchanganyiko

Dk. Gwajima atoa maelekezo kwa maofisa maendeleo nchini

Spread the love  WAZIRI wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii Jinsia Watoto,...

Habari Mchanganyiko

Kairuki awaweka mtegoni wakurugenzi watakaoshindwa kufikia malengo ya makusanyo

Spread the loveWAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na...

error: Content is protected !!