Wednesday , 1 May 2024
Home Kitengo Michezo Ishara ya kidole cha mwisho kumponza Mourinho
Michezo

Ishara ya kidole cha mwisho kumponza Mourinho

Jose
Spread the love

KOCHA mkuu wa Manchester Unite Jose Mourinho yupo katika wakati mgumu tena baada ya Chama cha Mpira wa Miguu England (FA) kumchunguza kufuatia kuonesha ishara ya kidole cha mwisho mara baada ya kumalizika kwa mchezo wa ligi kuu uliopigwa Old Trafford na kuibuka na ushindi wa mabao 3-1 dhidi ya Newcastle United. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea)

Mourinho alionesha ishara hiyo alipokuwa akitoka uwanjani mara baada ya kukamilika kwa mchezo huo huku akiwa anatamka maneno kwa lugha ya kireno ambayo yaliyo tafsiliwa na kuonekana kama matusi yalionekana kuwalenga magwiji wa klabu hiyo Paul Scholes na Rio Ferdinand ambao walinukuliwa wakisema kocha huyo anahalibu timu hiyo.

Hata alipoulizwa na waandishi wa habari nini maana ya kuonesha ishara ile, alisema kile ni kidole tu na ndio kifupi kuliko vyote.

Hii ni mara ya tatu kwa kocha huyo kuoneasha ishara hiyo ya kidole katika matukio tofauti, alionekana akifanya hivyo kwenye mchezo wa Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Valencia uliomalizika kwa sare ya bila kufungana na mara ya pili akiwa kwenye gari yake binafsi na kwenye mchezo uliopita wa Ligi Kuu England dhidi ya Newcastle.

Kocha huyo amekuwa katika wakati mgumu wa kunusuru kibarua chake ndani ya klabu hiyo kutokana na kuwa na mwenendo mbovu wa matokeo huku sababu kubwa ikiwa ni migogoro na wachezaji sambamba na mkurugenzi wa timu hiyo Ed Woodward ambaye alikataa kumpa fedha za kutosha kwenye dirisha la usajili.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

Michezo

Usiku wa Ulaya umerejea kibabe kabisa

Spread the love  LIGI ya Mabingwa barani Ulaya imerejea tena na awamu...

Habari MchanganyikoMichezo

Mambo ya Ndani, Ulinzi zang’ara michezo ya Mei Mosi Arusha

Spread the loveRais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA), Tumaini...

Michezo

Beti na Meridianbet mechi za leo

Spread the love IKIWA leo hii ni Jumapili tulivu kabisa, Meridianbet wanamkwambia...

error: Content is protected !!