Monday , 11 December 2023
Home Gazeti Habari za Siasa Mch. Msigwa apigwa ‘stop’ kufanya mikutano Iringa
Habari za SiasaTangulizi

Mch. Msigwa apigwa ‘stop’ kufanya mikutano Iringa

Mch. Peter Msigwa
Spread the love

JESHI la Polisi mkoani Iringa limempiga marufuku Mbunge wa Iringa Mjini, Peter Msigwa kufanya mikutano ya hadhara kwa madai ya kutoa lugha za matusi na uchochezi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kwa mujibu wa barua iliyosambaa mitandaoni inayodaiwa kutoka kwa Jeshi la Polisi Wilaya ya Iringa na kusainiwa na Kamanda wa Polisi wilayani humo, Yohana Mjengi, inadai kuwa Msigwa amekiuka makubaliano ya kibali alichopewa cha kufanya mikutano hiyo.

Barua hiyo inaeleza kuwa, Katika barua yake ya maombi, Msigwa aliomba kufanya mikutano ya hadhara katika kata mbalimbali, kwa ajili ya kukutana na wananchi, kupokea kero, kuhamasisha maendeleo na kupokea maoni kabla kwenda bungeni.

Lakini, barua hiyo inadai kuwa, Msigwa katika mkutano wake wa hadhara alioufanya kwenye kata ya Kihesa, alitoa maneno ya kashfa na uchochezi yanayoashiria uvunjifu wa amani kwenye jimbo lake na kwamba kwa mantiki hiyo haruhusiwi kuendelea na mikutano yake, hivyo kama akikaidi agizo hilo hatua kali za kisheria zitachukuliwa mara moja dhidi yake.

received_155963048681709

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Jaji Kiongozi akerwa wananchi kukosa imani na mahakama

Spread the loveWATENDAJI wa Mahakama ya Tanzania, wametakiwa kuweka mikakati itakayosaidia kurejesha...

BurudikaHabari za Siasa

Samia amchangia Professa Jay mil. 50, Chadema, wasanii wamwaga manoti

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amechangia kiasi cha Sh 50 milioni...

Habari za Siasa

Biteko: Samia ni muumini wa maridhiano sio kwa kuigiza

Spread the loveNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto Biteko...

Habari za SiasaTangulizi

Dk. Mpango: Sitakufa bali nitaishi

Spread the loveMAKAMU  wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk....

error: Content is protected !!