Wednesday , 8 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Kangi Lugola atengua uamuzi wake mwenyewe
Habari za Siasa

Kangi Lugola atengua uamuzi wake mwenyewe

Spread the love

SERIKALI imefuta utaratibu wa utoaji vibali kwa wananchi wanaolima jirani na kambi za wakimbizi. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Katazo hilo limetolewa jana na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Kangi Lugola katika mkutano wa hadhara na wananchi wa Wilaya ya Kankonko mkoani Kigoma baada ya kupokea malalamiko kutoka wananchi hao, kwamba utaratibu huo kuchelewesha shughuli zao.

Kufuatia malalamiko hayo, Waziri Lugola aliwataka wananchi wanaolima jirani na kambi za wakimbizi kuendelea na shughuli za kilimo pasipo kuomba kibali kama ilivyokuwa awali.

“Naagizia huu utaratibu ufutwe na wananchi wawe huru kwenda kulima katika maeneo ambayo yapo jirani na hiyo kambi pamoja na kambi zinginezo, na pia wasisumbuliwe na mtu yeyote, ” alisema Lugola.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Rais Samia: Matumizi ya nishati safi sio anasa, ladha ipo

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amesema matumizi ya nishati safi kwa...

Habari za SiasaTangulizi

Samia: Kuanzia Agosti marufuku kutumia mkaa, kuni

Spread the loveRAIS Samia Suluhu Hassan amemuagiza Waziri wa Nchi, Ofisi ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mwendokasi Kigogo – Segerea kujengwa awamu ya 5

Spread the loveNaibu Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (TAMISEMI), Festo Dugange...

Habari za SiasaMakala & Uchambuzi

Rais Samia ni Mzanzibari: Shida Iko Wapi?

Spread the loveTAIFA linakabiliwa na upungufu wa fikra sahihi. Upungufu huu unaonekana...

error: Content is protected !!