Thursday , 25 April 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndumbalo ateuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje
Habari za SiasaTangulizi

Ndumbalo ateuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje

Spread the love

RAIS John Magufuli amemteua Mbunge wa Songea Mjini, Dk. Damas Ndumbaro kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Dk. Susan Kolimba. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Dk. Ndumbalo anachukua nafasi ya Dk. Susan ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo tarehe 26 Septemba 2018 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Vile vile, taarifa hiyo inaeleza kuwa, Rais Magufuli amemteua Dkt. Faraji Mnyepe kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akichukua nafasi ya Prof. Adolf Mkenda ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.

Prof. Mkenda amechukua nafasi ya Meja Jenerali Mstaafu, Gaudence Milanzi ambaye amestaafu.

“Uteuzi wa viongozi hao umeanza leo tarehe 26 Septemba, 2018 na tarehe ya kuapishwa kwao itatangazwa baadaye,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Kilosa yawa mfano wa kuigwa miradi ya Mwenge nchini

Spread the love  KIONGOZI wa Mbio za Mwenge Kitaifa Godfrey Mzava amezitaka...

Habari za SiasaTangulizi

Biteko ataja vipaumbele 7 bajeti nishati 2024/25

Spread the love  NAIBU Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Dk. Doto...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mwekezaji amwaga bil. 39 kujenga viwanda 3 vya uchenjuaji

Spread the loveKampuni ya Mineral Access System Limited (MAST) inayoiwakilishwa kampuni ya...

Habari za SiasaTangulizi

Mpwa wa Magufuli mbaroni kwa kusambaza picha za utupu

Spread the loveJESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam limewakamata...

error: Content is protected !!