Thursday , 2 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Ndumbalo ateuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje
Habari za SiasaTangulizi

Ndumbalo ateuliwa kuwa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje

Spread the love

RAIS John Magufuli amemteua Mbunge wa Songea Mjini, Dk. Damas Ndumbaro kuwa Naibu Waziri wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, nafasi iliyokuwa inashikiliwa na Dk. Susan Kolimba. Anaripoti Regina Kelvin … (endelea).

Dk. Ndumbalo anachukua nafasi ya Dk. Susan ambaye uteuzi wake umetenguliwa.

Taarifa ya mabadiliko hayo imetolewa leo tarehe 26 Septemba 2018 na Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais Ikulu.

Vile vile, taarifa hiyo inaeleza kuwa, Rais Magufuli amemteua Dkt. Faraji Mnyepe kuwa Katibu Mkuu wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akichukua nafasi ya Prof. Adolf Mkenda ambaye ameteuliwa kuwa Katibu Mkuu Wizara ya Maliasili na Utalii.

Prof. Mkenda amechukua nafasi ya Meja Jenerali Mstaafu, Gaudence Milanzi ambaye amestaafu.

“Uteuzi wa viongozi hao umeanza leo tarehe 26 Septemba, 2018 na tarehe ya kuapishwa kwao itatangazwa baadaye,” inaeleza sehemu ya taarifa hiyo.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za SiasaTangulizi

Serikali yaanza msako wanaotoa mikopo kausha damu

Spread the loveSERIKALI imeanza kufuatilia watu, vikundi na taasisi zinazotoa kinyume cha...

Habari za Siasa

Spika Tulia aibana Serikali mafao ya wastaafu Jumuiya ya Afrika Mashariki

Spread the loveSPIKA wa Bunge, Dk. Tulia Ackson ameitaka Serikali kufanya tathimini...

Habari za Siasa

Serikali yawapa maagizo Ma-RC udhibiti magonjwa yasiyoambukiza

Spread the loveWAKUU wa mikoa nchini wametakiwa kuandaa utaratibu wa kuwawezesha wananchi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!