Friday , 3 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Fredrick Sumaye aviponda viwanda vya Magufuli
Habari za SiasaTangulizi

Fredrick Sumaye aviponda viwanda vya Magufuli

Spread the love

WAZIRI Mstaafu wa Jamhuri ya Muungano, Fredrick Sumaye amesema, nchi kwa sasa inaendeshwa “kiholela,” na kudai kuwa ikiwa chama chake kitafanikiwa kushika madaraka, kitaimarisha uchumi. Anaripoti Saed Kubenea … (endelea).

Amedai kuwa kwa sasa, uchumi wa taifa unaporomoka na kwamba serikali inayoongozwa na Rais John Pombe Magufuli, “imeamua kwa makusudi kuvuruga uchumi.”

“…huwezi kuzungumzia viwanda wakati uchumi umelemaa. Ndio maana hivi sasa, mtu anamiliki vyerahani vinne, lakini anaambiwa anamili kiwanda,” ameeleza.

Amesema, “tunajidanganya. Hatuwezi kuzungumzia viwanda bila kuwapo uchumi; na kwamba uchumi wenyewe ndio viwanda.”

Sumaye ametoa kauli hiyo leo Jumanne jijini Dar es Saalaam, wakati wa uzinduzi wa “sera mpya” za Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Amesema, kila anayetaka urais, sharti aeleze wananchi sera zake na ataifanyia nini nchi hii. Chadema kinazindua sera hizo ambazo zitapelekwa kwa wananchi na kunadiwa.

Sumaye amekuwa waziri mkuu kwa muda wa miaka kumi mfululizo katika kipindi cha utawala wa Benjamin Mkapa.

Katika kipindi cha uongozi wake, uchumi wa nchi ambao ulikuwa hoi kutokana na kutengwa na mashirika ya kimataifa – Benki ya Dunia (WB) na Shirika la Fedha la Kimataifa (IFM) , uliimarika kwa kasi.

Aidha, ni katika kipindi hicho, mfumuko wa bei ulipungua, ajira zilipatikana, elimu imeboreshwa na hospitali zote zilikarabatiwa na kuwa na dawa.

Katika hafla hiyo iliyohudhuriwa na watu mbalimbali, akiwamo mwakilishi wa ubalozi wa Marekani nchini, Chadema kimesema, kimeamua kuchukua hatua hiyo ili kujitofautisha na chama kilichopo madarakani.

Naye Freeman Mbowe, mwenyekiti wa chama hicho taifa amesema, sera ya Chadema ya sasa imezingatia namna ya uboreshaji wa uchumi.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari za Siasa

Serikali yasaka bilioni 3 kujenga daraja Mto Mpiji

Spread the loveSerikali imesema inaendelea na juhudi za kutafuta fedha kiasi cha...

Habari za SiasaTangulizi

Chadema kwafukuta kisa chaguzi, Lissu aibua tuhuma nzito

Spread the loveCHAGUZI za kusaka viongozi wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo...

Habari MchanganyikoTangulizi

Kimbunga “HIDAYA” chaendelea kuimarika, wananchi wapewa tahadhari

Spread the loveMAMLAKA ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA) inaendelea kutoa taarifa...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Chadema waendelea kulilia katiba mpya

Spread the loveCHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), kimeendelea kudai upatikanaji wa...

error: Content is protected !!