Saturday , 27 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Waliofariki MV Nyerere wafika 94
Habari MchanganyikoTangulizi

Waliofariki MV Nyerere wafika 94

Spread the love

IDADI ya watu waliofariki dunia katika ajali ya kivuko cha MV. Nyerere katika Ziwa Victoria jana. Anaripoti Mwandishi Maalum … (endelea).

Mpaka kufika saa 4 leo asubuhi pekee wameopolewa maiti 50 ambapo jioni jumla ya maiti 44 waliopolewa.

Watu 40 wanaripotiwa kuokolewa wakiwa hai mpaka sasa na wanaendele na matibabu.

John Mongella, Mkuu wa Mkoa wa Mwanza anasema, utafutaji wa miili mingine unaendelea.

Viongozi mbalimbali wapo eneo la tukio wakiendelea na harakati za uokoaji.

Miili ya maiti hao imehifadhiwa kwenye Kituo cha Afya cha Bwisya kwa mujibu wa Mongella.

Kivuko cha MV. Nyerere kilizama jana ziwani humo ikiwani kilomita 50 kabla ya kutia nanga kwenye Kisiwa cha Ukara ilipokuwa ikielekea.

Raila Odinga, Kiongozi wa upinzani wa muungano wa NASA nchini Kenya amemtumia salama za pole Rais wa Tanzania na Wananchi wote kutokana na ajali ya MV. nyerere.

“Naomboleza na raia wa Tanzania katika kipindi hiki kigumu. Mungu awape amani na utulivu…” ameandika Odinga katika ukurasa wake wa Facebook.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoTangulizi

Jacob, Malisa waachiwa kwa masharti

Spread the love  JESHI la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam,...

Habari za SiasaKimataifaTangulizi

Tanzania, Somalia kuibua maeneo mapya ya ushirikiano

Spread the love  RAIS Dk. Samia Suluhu Hassan, amesema Tanzania na Somalia...

Habari Mchanganyiko

Polisi wakanusha kufanya uzembe ajali iliyouwa mwandishi Ayo Tv

Spread the loveJESHI la Polisi limekanusha tuhuma zilizoibuliwa dhidi yake  kwamba limekawia...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia kuzindua gazeti litakalotoa habari za wafanyakazi Tanzania

Spread the loveSHIRIKISHO la Vyama vya Wafanyakazi Tanzania (TUCTA), liko mbioni kufufua...

error: Content is protected !!