Thursday , 2 May 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwalimu aliyemuua mwanafunzi afikishwa mahakamani
Habari Mchanganyiko

Mwalimu aliyemuua mwanafunzi afikishwa mahakamani

Spread the love

MWALIMU Respicius Patrick Mtazangira na Julieth Gerald wa Shule ya Msingi Kibeta iliyoko Manispaa ya Bukoba wanaotuhumiwa kumuua kwa viboko mwanafunzi wa darasa la tano, Sperius Eradius (13) wa shule hiyo, wamefikishwa mahakamani na Jeshi la Polisi mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Walimu hao wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Bukoba na kusomewa mashtaka yanayowakabili asubuhi ya leo tarehe 3 Septemba 2018 .

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya tukio hilo tarehe 27 Agosti mwaka huu, ambapo Mwalimu Mtazangira ambaye ni mwalimu wa nidhamu katika Shule ya Msingi Kibeta alimwadhibu na kupelekea kifo cha mwanafunzi huyo baada ya kumpokea mizigo mwalimu wake Julieth Gerald na baadae kutuhumiwa kuiba pochi ya mwalimu huyo.

Mwanafunzi huyo alizikwa tarehe 31 Agosti, 2018 katika kijiji cha Kitoko kilichoko Kata ya Mubunda wilayani Muleba mkoani Kagera.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

Equity Bank yaendelea kusotea mabilioni ya fedha mahakama rufani

Spread the loveBENKI za Equity ya Tanzania na Kenya, zimeendelea kupambana mahakamani...

Habari Mchanganyiko

NEMC yatoa elimu matumizi sahihi ya zebaki kwa wachimbaji

Spread the loveBARAZA la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC)...

BiasharaHabari Mchanganyiko

Oryx gesi yagawa mitungi, majiko 100 kwa waandishi wa habari Dar

Spread the loveKAMPUNI ya Oryx Gesi Tanzania imegawa mitungi 100 ya gesi...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Mavunde ataja malengo “Vision 2030”

Spread the loveWAZIRI wa Madini amesema dhana ya “Vision 2030” inakusudia kuiendeleza...

error: Content is protected !!