Friday , 19 April 2024
Home Habari Mchanganyiko Mwalimu aliyemuua mwanafunzi afikishwa mahakamani
Habari Mchanganyiko

Mwalimu aliyemuua mwanafunzi afikishwa mahakamani

Spread the love

MWALIMU Respicius Patrick Mtazangira na Julieth Gerald wa Shule ya Msingi Kibeta iliyoko Manispaa ya Bukoba wanaotuhumiwa kumuua kwa viboko mwanafunzi wa darasa la tano, Sperius Eradius (13) wa shule hiyo, wamefikishwa mahakamani na Jeshi la Polisi mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Walimu hao wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Bukoba na kusomewa mashtaka yanayowakabili asubuhi ya leo tarehe 3 Septemba 2018 .

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya tukio hilo tarehe 27 Agosti mwaka huu, ambapo Mwalimu Mtazangira ambaye ni mwalimu wa nidhamu katika Shule ya Msingi Kibeta alimwadhibu na kupelekea kifo cha mwanafunzi huyo baada ya kumpokea mizigo mwalimu wake Julieth Gerald na baadae kutuhumiwa kuiba pochi ya mwalimu huyo.

Mwanafunzi huyo alizikwa tarehe 31 Agosti, 2018 katika kijiji cha Kitoko kilichoko Kata ya Mubunda wilayani Muleba mkoani Kagera.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari Mchanganyiko

NMB Pesa Akaunti yawavutia wakaguzi wa ndani Afrika

Spread the loveUbunifu wa bidhaa bora wa Benki ya NMB pamoja na...

Habari Mchanganyiko

Carbon First, Ruangwa wasaini makubaliano ya biashara ya hewa ukaa

Spread the love  KAMPUNI ya Carbon First Tanzania Limited na Halmashauri ya...

Habari Mchanganyiko

CBE yawakumbuka wenye mahitaji maalum Jangwani

Spread the loveCHUO cha Elimu ya Biashara (CBE), kimetoa msaada mbalimbali na...

Habari Mchanganyiko

Mume auwa mke kwa kumchoma visu, ajisalimisha Polisi

Spread the loveJACKSON Kalamji (49), anashikiliwa na Jeshi la Polisi jijini Mwanza,...

error: Content is protected !!