Wednesday , 27 September 2023
Home Habari Mchanganyiko Mwalimu aliyemuua mwanafunzi afikishwa mahakamani
Habari Mchanganyiko

Mwalimu aliyemuua mwanafunzi afikishwa mahakamani

Spread the love

MWALIMU Respicius Patrick Mtazangira na Julieth Gerald wa Shule ya Msingi Kibeta iliyoko Manispaa ya Bukoba wanaotuhumiwa kumuua kwa viboko mwanafunzi wa darasa la tano, Sperius Eradius (13) wa shule hiyo, wamefikishwa mahakamani na Jeshi la Polisi mkoani Kagera. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Walimu hao wamefikishwa katika mahakama ya wilaya ya Bukoba na kusomewa mashtaka yanayowakabili asubuhi ya leo tarehe 3 Septemba 2018 .

Watuhumiwa hao wanadaiwa kufanya tukio hilo tarehe 27 Agosti mwaka huu, ambapo Mwalimu Mtazangira ambaye ni mwalimu wa nidhamu katika Shule ya Msingi Kibeta alimwadhibu na kupelekea kifo cha mwanafunzi huyo baada ya kumpokea mizigo mwalimu wake Julieth Gerald na baadae kutuhumiwa kuiba pochi ya mwalimu huyo.

Mwanafunzi huyo alizikwa tarehe 31 Agosti, 2018 katika kijiji cha Kitoko kilichoko Kata ya Mubunda wilayani Muleba mkoani Kagera.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Kapinga: Usambazaji umeme vijijini mwisho Desemba 2023

Spread the love  NAIBU Waziri wa Nishati, Judith Kapinga, amesema ifikapo mwezi...

Habari Mchanganyiko

Wizara ya madini kurusha ndege ya utafiti wa madini Geita

Spread the loveKutokana na mchango wa wachimbaji wadogo wa madini kwenye pato...

Habari Mchanganyiko

Jafo aagiza kampuni za madini kuzingatia utunzaji mazingira, azitaka zijifunze kwa GGML

Spread the loveWAZIRI wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na...

Habari Mchanganyiko

Rais Samia apewa tano ujenzi barabara Mtwara

Spread the loveWANANCHI wa Mkoa wa Mtwara, wameishukuru Serikali ya Rais Dk....

error: Content is protected !!