Monday , 6 May 2024
Home Gazeti Habari za Siasa Dada wa Rais Magufuli azikwa Chato
Habari za Siasa

Dada wa Rais Magufuli azikwa Chato

Spread the love

MWILI wa Monica Magufuli, dada wa Rais John Magufuli umezikwa leo tarehe 21 Agosti mwaka huu, nyumbani kwao katika kijiji cha Mlimani Chato mkoani Geita. Anaripoti Mwandishi Wetu … (endelea).

Kabla ya mwili huo kuzikwa, ilitangulia misa takatifu ya kumuombea marehemu Monica iliyoongozwa na Baba Askofu Mkuu Mwandamizi, Yuda Thaddeus Ruwaichi.

Baada ya misa hiyo, Rais Magufuli aliwaongoza mamia ya watu waliojitokeza kumzika marehemu dada yake Monica aliyefariki dunia tarehe 19 Agosti, 2018 katika hospitali ya Bugando jijini Mwanza alikokuwa napatwa matibabu.

Viongozi mbalimbali wa serikali na wastaafu washiriki mazishi ya marehemu Monica, wakiwemo, Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi John Kijazi, Rais Mstaafu wa awamu ya tatu, Benjamin Mkapa, Rais Mstaafu wa awamu ya nne, Dkt. Jakaya Kikwete na Waziri Mkuu Mstaafu wa Kenya, Raila Odinga.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

BiasharaHabari za Siasa

Bunge laitaka Serikali kudhibiti ufisadi miradi ya mkakati

Spread the loveKAMATI ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu, imeitaka Serikali kuimarisha...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Wizara ya Uchukuzi yaomba kuongezewa bajeti na Bunge

Spread the loveWIZARA ya Uchukuzi imeliomba Bunge liidhinishe bajeti yake kwa mwaka...

Habari MchanganyikoHabari za Siasa

Serikali kutafuta mwekezaji mwingine Bandari ya Dar es Salaam

Spread the loveSERIKALI inaendelea kutafuta mwekezaji mwingine atakayeendesha gati namba nane hadi...

Habari za SiasaTangulizi

Kinana: Hatukubali kushutumiwa kwa uongo

Spread the loveMakamu Mwenyekiti wa CCM Bara, Abdulrahman Kinana amesema viongozi wa...

error: Content is protected !!