Sunday , 5 May 2024
Home Kitengo Michezo Salah mikononi kwa Polisi
Michezo

Salah mikononi kwa Polisi

Spread the love

MSHAMBULIAJI wa Liverpool na timu ya taifa ya Misri, Mohammed Salah ameingia matatizoni na polisi wa Merseyside baada ya kuibuka kwa video mitandaoni akionekana kuendesha gari huku akiwa anatumia simu yake ya mkononi. Anaripoti Kelvin Mwaipungu … (endelea).

Polisi jijini Liverpool wamethibitisha tukio hilo kupitia ukurasa wao unaopatikana kwenye mtandao wa twitter na kusema kwamba video hiyo imekabidhiwa kwenye kitengo husika.

Video hiyo ambayo ilisambaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonesha mchezaji huyo akiwa anatumia simu yake huku akiwa amesimamisha gari lake kwa muda baada ya kuzingirwa na mashabiki wakiwemo watoto, kisha akaamua kuondoa gari akiwa bado anatumia simu yake.

Hata hivyo uongozi wa klabu ya Liverpool ulitoa taarifa ya kuwa imewafahamisha polisi wa Merseyside kuhusu video hiyo baada ya kushauriana na mchezaji mwenyewe na kujua nini kilitokea wakati tukio hilo linafanyika.

Leave a comment

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

Related Articles

Michezo

Usiishie kuangalia tu game za leo, piga na mkwanja na Meridianbet

Spread the love  LIGI mbalimbali barani ulaya zitarejea tena Jumamosi ya leo...

Michezo

Ligi mbalimbali za pesa kuendelea leo

Spread the love Ijumaa ya leo ambapo mechi mbalimbali zinaendelea Duniani Meridianbet...

Michezo

Europa na Conference kukupatia pesa ndefu leo

Spread the love  ALHAMISI ya leo tutaenda kushuhudia mitanange ya kukata na...

Habari MchanganyikoMichezo

Wanamichezo Mei Mosi wachangia wahitaji vitu vya mil. 11.5

Spread the loveWanamichezo wanaoshiriki Michezo ya Mei Mosi Taifa 2024 jijini Arusha...

error: Content is protected !!